Mimi ni Freddy Macha. Mwandishi na Mwanamuziki. Nyumbani Bongo huandika safu mbili, moja Mwananchi , kwa Kiswahili, kila Jumapili, nyingine The Citizen (Kimombo) kila Ijumaa. Nahusudu michezo, afya, lugha, sanaa, fasihi na kuukomboa ulimwengu dhidi ya ujinga, umaskini na maradhi. Ukitaka habari zangu zaidi cheki: www.freddymacha.com. Au soma blogu ya Kiingereza : http://freddymacha.blogspot.com….
Kazi zako nyingi sana Freddy na umeamua kujitoa hasa.Kweli kabisa unajitolea sana.Nimevutiwa sana na vitu unavyopendelea kama vile michezo,afya,lugha,sanaa,fasihi na kuukomboa ulimwengu dhidi ya ujinga,umasikini na maradhi.Lakini naona kuna vitu kama umevisahau pia!Ni kweli kuwa unatoka Bongo na unaandikia Mwananchi Jumapili na The Guardian kila Jumanne.Wewe ni muelimishaji lakini kwa maonio yangu naona umesahau kitu moja au mojawapo ya mambo haya hapa katika utambulisho wako wa wewe ni nani?Kuwa unaelimisha jamii pia kutoka katika maradhi ya demakrasia,ufisadi,ubabe,unyang’anyi na uporaji wa haki za wanyonge hasahasa katika bara letu au nchi zetu hizi za Afrika ambako kwa kweli bado inaonekana kuwa demakrasia bado ni ndoto kubwa kuja kutokea.
Kwamba tatizo la hapa kwetu ni kuwa hata wale walio nje ya kinyang’nyilo wakiingia na wao pia kutoka ni vigumu sana!Afrika tutatoka?Itachukua muda sana.
Kabla ya yote kwanza pokea heshima yako shikamoo,mimi ni mmoja kati ya watu wanaopenda kusoma makala zako,binafsi navutiwasana na makala zako kwasababu najifunza mengi kutokana nazo hasa yale yanayoendelea huko ughaibuni,pianafurahi sana unapoandika kuhusu afya,mazoezi na mambo wanayofanya wabongo wanaoishi huko.Kwakweli napenda kukupongeza kwa juhudi zako za kutupasha yanayoendelea huko ulaya hasa yanayofanywa na wabongo huko.
Ninafurahishwa na makala zako. hasa ile ya mishipa ya PC.
na michapo ya majuu.
Si unajua sisi hatujavuka mipaka !
Andika zaidi kuhusu mishipa ya PC na Natural Therapies.
Naomba unielekeze chuo kizuri nichoweza kusoma kwa njia ya posta sio online. kuhusu Afya masomo nayopenda ni
Nutritional therapy, Bio- Mechanics.
Ahsante
nijibu kwa teshaernest@hotmail.com
mimi ni mpenzi sana wa nakala zako kutoka Mwananchi Jumapili!. I tend to Buy this gazeti only bse of your nakala. zinanipa uelewa zaidi kutoka nchi za mbali, maana mimi ni Mtanzania ambaye nipo Dar, pia ni mtu ambaye sijawahi kusafiri nchi za mbali but Mungu akipenda i wish nije kufanya mapumziko German! Napapenda German sana, japo nasikia kuwa wale watu wana roho za unyama. plz if u can naomba unipe japo walau maelezo ya huko
Cathy,
Nashukuru kwa usomaji na hoja zako.
Ingefaa uhudhurie semina zangu ambazo huongelea masuala kadhaa ikiwepo vile vile maisha ya ughaibuni. Hebu fuatilia gazeti la Lucky (jipya nchini) pia blogu kadhaa (hii yangu ya Kitoto) Michuzi, Kwanza Jamii (Maggid Mjengwa ) na Bongo Celebrity ambazo zitatangaza na zimekuwa zikitangaza semina hizi na zijazo.
Sasa…kujibu swali lako kuhusu Ujerumani.
Rahisi kwako ni kwenda mwenyewe na kujionea na kuishi kule. Maisha yeyote nje ya utamaduni wako huwa ya kutisha na kuchangamsha ; kutatiza na kufundisha. Si rahisi lakini pia yanakujenga ukawa mkakamavu sana kuhusiana na wewe ulivyo.
Wengine huwashinda; wengine huwajenga. Ujerumani ni uzunguni. Na kule kuna masharti magumu. La kwanza jifunze lugha yao mengine yatakuwia rahisi. Usipojifunza lugha utateseka sana. La pili utamaduni, tofauti hata na wa wazungu wengine (Wajerumani kiboko yao) la tatu hali ya hewa ….
Ah, hapa haitoshi kufafanua lakini jaribu kuhudhuria semina zijazo. Niandikie Email ntakutumia makala tulizotoa semina zilizopita…za Mei 2009.
kilimanjaro1967@hotmail.com
Asante kwa kuandika makala kuhusu “Tanzania: Sex And the Exploitation of Children”. Nimeisoma kupitia http://allafrica.com/stories/200809190580.html na nimei-blog kwenye http://ukumbi.wordpress.com/2008/09/21/tanzania-sex-and-the-exploitation-of-children/
Vp kaka?mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza shahada ya ualimu(Bed) hapa TUMAINI UNIVERSITY,MAKUMIRA UNIVERSITY COLLEGE, ARUSHA.Ninasoma sana makala zako na ninavutiwa nazo sana.
Endelea kutupa elimu isiyoisha utamu,kila siku.
kazi njema
valle
Kaka Fred, Mungu akubariki. Kazi yako nzuri na kwa kweli dunia inakutambua na Watanzania tunajivunia uwepo wako.
Endelea na kazi nzuri ya kuelimisha jamii, kupitia peni yako naamini watu wengi watafunguliwa na kuokoka ( in terms of education and knowledge).
Mgusii
Kaka Freddy, japo ni siku nyingi tangu tuwasiliane, huwa napitia kwenye anga zako na kupata hili na lile. Kimsingi kazi zako ni chema. Laiti wengi tungeiangalia jamii kwa jicho kali kama ufanyavyo, si haba tungeacha alama isiyofutika duniani.
Wengi wana elimu na taaluma, ima ni wachoyo wa kuitoa au wametekwa na maisha yao binafsi kiasi cha kuisahau jamii.
Kila la heri na ongeza bidii.
Sina cha kusema unatisha kaka mungu akipenda nitauzulia semina zako zijazo ukija bongo,nimesikia utakuja mwezi septemba napenda tuonane kwani nina mpango wa kuja kusoma LONDON waweza nisaidia hata kwa ushauri kaka,KAZI NJEMA MARA NYINGINE.
Tutawafahamisha kupitia vyombo vya habari. Usichoke kutazama blogu hii , ya akina Michuzi na Maggid Mjengwa tutatangaza. Pia waweza kutuma SmS unipe namba yako ya simu.
Freddy,kazi yako nimeikubali mzee!Kaza buti…Tunahitaji zaidi na zaidi mawazo yako na elimu uitowayo kupitia mziki,makala na vitabu.Ila ninaomba unifahamishe wapi nitapata na kala ya kitabu chako kiitwacho TWENZETU ULAYA.Nimesoma kitabu chako cha MPE MANENO YAKE.Kazi njema!
Tuko mbioni kutayarisha nakala mpya za Twenzetu Ulaya, kikishachapwa tena, Inshallah, tutawajulisha wadau, ahsante kwa kuulizia Mapuchila
Kwanza kabisa naomba nikupe heshima yako”Shikamoo”.Mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa jarida zako mbalimbali na naweza kusema kwamba nimejifunza mengi,sio mengi tu bali mengi sana kama vile jinsi ya kuishi na watu vizuri,umuhimu wa elimu na pia nimejifunza baadhi ya tamaduni za waingereza”KALAMU KUTOKA LONDON”.Kusema kweli nimejifunza mambo mengi sana ambayo sikuwahi kujifunza mahali popote pale na ninaweza nikasema ni zaidi ya elimu ya darasani.Kwaufupi unatuelimisha,burudisha na hata pia kututia moyo wa kufanya kazi kwa bidii,kaza buti na hongera sana kwa kazi nzuri na ya kupendeza.KAZI NJEMA…
Nashukuru Amani. Tuko pamoja…