Feeds:
Posts
Comments

Archive for the ‘Blogroll’ Category

Arusi za Waafrika Majuu huwa zina ugumu na urahisi wake.
Ugumu?
Mwafrika kuwa mbali na jamii na jamaa zake; akibahatika kupata wahudhuriaji wachache basi humshukuru Mungu. Ugenini ni ugenini tu…
Urahisi?
Ile furaha isiyopatikana kirahisi kutokana na kuishi ughaibuni  kama mgeni, huvimba, ikanepa na kuringa : raha ya kufanya kitendo maalum.
Karibuni nimehudhuria arusi mbili kem kem. Mosi,  ya  dada [...]

Read Full Post »

RAS NAS  ZIARANI NORWAY 2009
Mwanamuziki mkongwe wa miondoko ya rege na muziki wa dansi mwenye makao  Oslo, Norway, Ras Nas ( Nasibu Mwanukuzi),  anapanga safu kali kwa ajili ya ziara ya miji sita Norway. Ziara hiyo itakayoanza Kongsberg tarehe 23 Oktoba itamalizikia jijini Trondheim 7 Desemba.

Kikosi cha Ras Nas kinachanganya wanamuziki toka Congo Brazzaville, Ivory [...]

Read Full Post »

Mjadala aliopopoa Maggid ” Mwenyekiti”  Mjengwa (pichani, kulia, alipohudhuria semina zangu,  Dar, Mei)  blogu ya Kwanza Jamii umezua maoni kem kem.  Ni mjadala muhimu kwa sababu kadhaa:
1-Zamani Mwalimu Nyerere alisisitiza sana juu ya utaifa ndiyo maana akashauri sote tuongee Kiswahili. Hii imechangia sana kutokuwa na kero za ukabila Tanzania kama zilivyo nchi nyingi bara Afrika. [...]

Read Full Post »

Nasibu Mwanukuzi au anavyojulikana kwa jina la kisanii, Ras Nas…katoka na kibao ambacho pia ni  jina la Albam yake ya pili kinachoutukuza na kuughani mji wa  Dar es Salaam karibuni.
Moja ya magazeti  makubwa nchini humo: Dagsavisen liliipa albam hiyo nyota tano. Nyota tano si mchezo kwa mwanamuziki wa Kiafrika anayetumbuiza Uzunguni.
Niliwahi kufanya kazi na Nasibu Mwanukuzi [...]

Read Full Post »

JIANDIKISHE HARAKA….
Je wewe ni mwanablogu (Blogger) au mdau wa habari na mawasiliano kwa umma kwa kutumia mtandao? Kama jibu ni ndio, tafadhali unaombwa kujiorodhesha kwa ajili ya maandalizi ya Kongamano Maalumu la Kitaifa kwa ajili Wanablogu (Bloggers) na wadau wa habari na mawasiliano wa Tanzania (Tanzanians Bloggers Summit) linalotarajiwa kufanyika Desemba mwaka huu jijini Dar-es-salaam,Tanzania.
Dhumuni [...]

Read Full Post »

Jamii zetu zinazoendelea zinahitaji sana Elimu.  Elimu itakayotusaidia kupambana na maadui kama : kutojua kupanga muda (Time Management) tatizo linalotufanya tuchelewe, tusiwe na mpangilio wa maisha ; halafu, kutoyajali mazingira yetu (vyoo vichafu na kutupa taka ovyo).Wataalamu wameshatuonya kuwa makaratasi ya plastiki tunayoyaacha kiholela kila mahali (yenye madawa hatari) yanaharibu rutuba na uhai ; yatakaa ardhini miaka 500 !!!

Si [...]

Read Full Post »

Zoezi maalum la kusaidia mabega kutokana na kazi mbalimbali zinazoathiri migongo, shingo na kichwa. Kuning’iniza bega moja ukizungusha mkono pande zote, huku mkono mwingine umeshika kiti au meza. 
Semina zilitayarishwa na jarida la LUCKY linaloendeshwa kwa ushirikiano wa wananchi wanaojitolea mhanga kuelemisha na kuendeleza jamii ya Tanzania.  Waliosimamia kazi hii ni Innocent Swai na mhariri wake [...]

Read Full Post »

Karibuni nimeingia tena Bongo baada ya miaka miwili. Ama kweli kwa tunaoishi ughaibuni kurudi nyumbani ni kama kwenda hospitali. Kabla ya tiba lakini, shurti  kuujua ugonjwa.

Tiba ya kwanza utani, masihara na vicheko.  Hapa tuko Nyumba ya Sanaa (iliyofunguliwa na Mwalimu Nyerere mwaka 1983); leo imegeuzwa Jumba La Kila Kitu : baa, kamari, michezo, hoteli, mahali pa watalii kununua vito vya Tanzania, makutano kwa [...]

Read Full Post »

Karibu  ndani; karibu chakula….sikiliza  moja ya nyimbo zangu penzi unaoongelea  namna mbalimbali za Uhuru; … na jinsi Uhuru ulivyo muhimu kuliko kitu kingine chochote duniani.
Niliutunga mwaka 1980 wakati  bado naishi “geto” moja pale Mwananyamala Kisiwani, Dar es Salaam.  Usiku nilioupika sikulala kutokana na kilio cha mwanamke aliyekuwa akikandikwa makonde,  mateke, matusi na mumewe aliyemkuta kaomba Sabuni toka kwa jirani sababu [...]

Read Full Post »

“ELIMU HAINA MWISHO…”
Methali ya Kiswahili
 Nchi yetu ina utata.
Mheshimiwa Rais kachorwa vibaya mitandaoni; miezi kadhaa iliyopita akazomewa ilhali kachaguliwa kwa asilimia 80 ya kura; Rais wa zamani, bwana Mwinyi akapigwa kofi hadharani; ajali za mabasi zimezidi,uvutaji bangi (hasa miongoni mwa vijana) umefikia asilimia 90 sehemu fulani fulani; viongozi mafisadi mahakamani; utovu wa nidhamu unaiandama nchi [...]

Read Full Post »

Older Posts »