Said Ahmed Mohammed keshatoa zaidi ya vitabu 30 – Riwaya 11 (ikiwepo” Asali Chungu” kigongo chake cha kwanza kilichomwagika uwanjani mwaka 1976), Tamthiliya 7, mikusanyiko minne ya Ushairi na mikusanyiko Saba ya Hadithi fupi ambayo moja wapo ni “Kiti cha Moyoni” alichochangia na Ken Walibora na “Damu Nyeusi” (pia na Ken Walibora) kikatoka 2007. Mbali na vitabu, Profesa Said ambaye ni mhadhiri wa lugha za Kiafrika chuo kikuu cha Bayreuth, Ujerumani(toka 1997) na keshachapa vitabu vingi vya watoto wa shule za msingi ambavyo lengo lake kufundisha, kutukuza na kujenga lugha na fasihi ya Kiswahili.
Baadhi ya vitabu vyake Profesa Said Ahmed Mohammed – vyote vimechapishwa Kenya.
(more…)






