Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘Mike Sikawa’

Picha mbili toka Shule iliyotujenga kitabia ya Mzumbe,  mwaka 1973-74.

Ya kwanza  jioni moja kabla ya jua kutua mwaka 1974.  Kilikuwa kikundi cha mabondia. Kawaida shule za kulala za sekondari huwa na uchaguzi ambao enzi hizo tuliziita kwa Kizungu “hobby” ina maana burudani baada ya kazi au masomo.  Husaidia wewe kijana kusahau masomo magumu, kujifunza kitu chochote kinachokuongezea nidhamu na bidii ya elimu na kujiendeleza. Kitaifa miaka ya Sabini mwito uliopigiwa kelele na   TANU chini ya  Mwalimu Nyerere ulikuwa Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea. ..

Toka kushoto aliyenyoosha ngumi ni kijana aliyekuja kuwa msomi, mwanafikra, mwandishi wa vitabu (mathalan, Makuadi wa Soko Huria, E & D Limited, 2002) na mhadhiri maarufu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Chachage S. Chachage.

Enzi hizo tulimwita Seti. Alikuwa mchangamfu na alipendwa hadi alipokuja kuwa mtaalamu maarufu wa mambo ya elimu jamii nchini. Leo anakumbukwa kwa jina la Profesa Chachage. Alifariki mwaka 2006. (more…)

Read Full Post »

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.

Join 355 other followers