Mimi ni Freddy Macha. Mwandishi na Mwanamuziki. Nyumbani Bongo huandika safu mbili, Mwananchi , kwa Kiswahili, “Kalamu toka London,” kila Jumapili, nyingine The Citizen (Kiingereza) “Chat from London” kila Ijumaa. Nahusudu michezo, afya, lugha, sanaa, fasihi na kuukomboa ulimwengu dhidi ya ujinga, uongo, umaskini na maradhi.
Nikiwa na bendi ya Kitoto, mjini Bath, Uingereza, mwaka 1993…
(toka kushoto: Ife Tolentino(Brazil, besi), Douglas Melo(Brazil, Meneja ), Ingrid Laubrock (Ujerumani, Sax), Matt Hodgkins (Kanada, Drums) na miye, Freddy Macha (Tanzania, kuimba na gitaa).
Habari zangu zaidi angalia: www.freddymacha.com. Au soma blogu ya Kiingereza : http://freddymacha.blogspot.com….
Soma pia makala zangu kama ulizikosa magazetini :http://www.makalazangu.blogspot.com/
Kazi zako nyingi sana Freddy na umeamua kujitoa hasa.Kweli kabisa unajitolea sana.Nimevutiwa sana na vitu unavyopendelea kama vile michezo,afya,lugha,sanaa,fasihi na kuukomboa ulimwengu dhidi ya ujinga,umasikini na maradhi.Lakini naona kuna vitu kama umevisahau pia!Ni kweli kuwa unatoka Bongo na unaandikia Mwananchi Jumapili na The Guardian kila Jumanne.Wewe ni muelimishaji lakini kwa maonio yangu naona umesahau kitu moja au mojawapo ya mambo haya hapa katika utambulisho wako wa wewe ni nani?Kuwa unaelimisha jamii pia kutoka katika maradhi ya demakrasia,ufisadi,ubabe,unyang’anyi na uporaji wa haki za wanyonge hasahasa katika bara letu au nchi zetu hizi za Afrika ambako kwa kweli bado inaonekana kuwa demakrasia bado ni ndoto kubwa kuja kutokea.
Kwamba tatizo la hapa kwetu ni kuwa hata wale walio nje ya kinyang’nyilo wakiingia na wao pia kutoka ni vigumu sana!Afrika tutatoka?Itachukua muda sana.
Kabla ya yote kwanza pokea heshima yako shikamoo,mimi ni mmoja kati ya watu wanaopenda kusoma makala zako,binafsi navutiwasana na makala zako kwasababu najifunza mengi kutokana nazo hasa yale yanayoendelea huko ughaibuni,pianafurahi sana unapoandika kuhusu afya,mazoezi na mambo wanayofanya wabongo wanaoishi huko.Kwakweli napenda kukupongeza kwa juhudi zako za kutupasha yanayoendelea huko ulaya hasa yanayofanywa na wabongo huko.
Ninafurahishwa na makala zako. hasa ile ya mishipa ya PC.
na michapo ya majuu.
Si unajua sisi hatujavuka mipaka !
Andika zaidi kuhusu mishipa ya PC na Natural Therapies.
Naomba unielekeze chuo kizuri nichoweza kusoma kwa njia ya posta sio online. kuhusu Afya masomo nayopenda ni
Nutritional therapy, Bio- Mechanics.
Ahsante
nijibu kwa teshaernest@hotmail.com
mimi ni mpenzi sana wa nakala zako kutoka Mwananchi Jumapili!. I tend to Buy this gazeti only bse of your nakala. zinanipa uelewa zaidi kutoka nchi za mbali, maana mimi ni Mtanzania ambaye nipo Dar, pia ni mtu ambaye sijawahi kusafiri nchi za mbali but Mungu akipenda i wish nije kufanya mapumziko German! Napapenda German sana, japo nasikia kuwa wale watu wana roho za unyama. plz if u can naomba unipe japo walau maelezo ya huko
Cathy,
Nashukuru kwa usomaji na hoja zako.
Ingefaa uhudhurie semina zangu ambazo huongelea masuala kadhaa ikiwepo vile vile maisha ya ughaibuni. Hebu fuatilia gazeti la Lucky (jipya nchini) pia blogu kadhaa (hii yangu ya Kitoto) Michuzi, Kwanza Jamii (Maggid Mjengwa ) na Bongo Celebrity ambazo zitatangaza na zimekuwa zikitangaza semina hizi na zijazo.
Sasa…kujibu swali lako kuhusu Ujerumani.
Rahisi kwako ni kwenda mwenyewe na kujionea na kuishi kule. Maisha yeyote nje ya utamaduni wako huwa ya kutisha na kuchangamsha ; kutatiza na kufundisha. Si rahisi lakini pia yanakujenga ukawa mkakamavu sana kuhusiana na wewe ulivyo.
Wengine huwashinda; wengine huwajenga. Ujerumani ni uzunguni. Na kule kuna masharti magumu. La kwanza jifunze lugha yao mengine yatakuwia rahisi. Usipojifunza lugha utateseka sana. La pili utamaduni, tofauti hata na wa wazungu wengine (Wajerumani kiboko yao) la tatu hali ya hewa ….
Ah, hapa haitoshi kufafanua lakini jaribu kuhudhuria semina zijazo. Niandikie Email ntakutumia makala tulizotoa semina zilizopita…za Mei 2009.
kilimanjaro1967@hotmail.com
Asante kwa kuandika makala kuhusu “Tanzania: Sex And the Exploitation of Children”. Nimeisoma kupitia http://allafrica.com/stories/200809190580.html na nimei-blog kwenye http://ukumbi.wordpress.com/2008/09/21/tanzania-sex-and-the-exploitation-of-children/
Vp kaka?mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza shahada ya ualimu(Bed) hapa TUMAINI UNIVERSITY,MAKUMIRA UNIVERSITY COLLEGE, ARUSHA.Ninasoma sana makala zako na ninavutiwa nazo sana.
Endelea kutupa elimu isiyoisha utamu,kila siku.
kazi njema
valle
Kaka Fred, Mungu akubariki. Kazi yako nzuri na kwa kweli dunia inakutambua na Watanzania tunajivunia uwepo wako.
Endelea na kazi nzuri ya kuelimisha jamii, kupitia peni yako naamini watu wengi watafunguliwa na kuokoka ( in terms of education and knowledge).
Mgusii
Kaka Freddy, japo ni siku nyingi tangu tuwasiliane, huwa napitia kwenye anga zako na kupata hili na lile. Kimsingi kazi zako ni chema. Laiti wengi tungeiangalia jamii kwa jicho kali kama ufanyavyo, si haba tungeacha alama isiyofutika duniani.
Wengi wana elimu na taaluma, ima ni wachoyo wa kuitoa au wametekwa na maisha yao binafsi kiasi cha kuisahau jamii.
Kila la heri na ongeza bidii.
Sina cha kusema unatisha kaka mungu akipenda nitauzulia semina zako zijazo ukija bongo,nimesikia utakuja mwezi septemba napenda tuonane kwani nina mpango wa kuja kusoma LONDON waweza nisaidia hata kwa ushauri kaka,KAZI NJEMA MARA NYINGINE.
Tutawafahamisha kupitia vyombo vya habari. Usichoke kutazama blogu hii , ya akina Michuzi na Maggid Mjengwa tutatangaza. Pia waweza kutuma SmS unipe namba yako ya simu.
Freddy,kazi yako nimeikubali mzee!Kaza buti…Tunahitaji zaidi na zaidi mawazo yako na elimu uitowayo kupitia mziki,makala na vitabu.Ila ninaomba unifahamishe wapi nitapata na kala ya kitabu chako kiitwacho TWENZETU ULAYA.Nimesoma kitabu chako cha MPE MANENO YAKE.Kazi njema!
Tuko mbioni kutayarisha nakala mpya za Twenzetu Ulaya, kikishachapwa tena, Inshallah, tutawajulisha wadau, ahsante kwa kuulizia Mapuchila
Kwanza kabisa naomba nikupe heshima yako”Shikamoo”.Mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa jarida zako mbalimbali na naweza kusema kwamba nimejifunza mengi,sio mengi tu bali mengi sana kama vile jinsi ya kuishi na watu vizuri,umuhimu wa elimu na pia nimejifunza baadhi ya tamaduni za waingereza”KALAMU KUTOKA LONDON”.Kusema kweli nimejifunza mambo mengi sana ambayo sikuwahi kujifunza mahali popote pale na ninaweza nikasema ni zaidi ya elimu ya darasani.Kwaufupi unatuelimisha,burudisha na hata pia kututia moyo wa kufanya kazi kwa bidii,kaza buti na hongera sana kwa kazi nzuri na ya kupendeza.KAZI NJEMA…
Nashukuru Amani. Tuko pamoja…
Asante kaka kwa kunifanya kupenda kusoma gazeti la mwananchi kila jumapili.
Makala zako zimekuwa msaada tosha kwa wanaopenda kujifunza kwani sisi wabongo ni mahodari wa kusoma ila wagumu wa kuelewa ndio maana maprofesa kibao lakini maendeleo ziro.
Asante kaka Mungu akubariki endelea kutuelemisha japo sisi wenyewe wagumu.
Big up kaka
Hata mimi huwa nasoma sana vitu vyako hapa newsroom ya Mwananchi japo ni PHOTOJOURNALIST lakini si haba nazipitia kwa sana.Kaza uzi
Pole kwa kazi nzito kaka yangu,pia napenda kukupongeza kwa kazi nzuri uifanyao hasa katika kutoa hamasha na kuikomboa Africa na dunia kwa ujumla,nafarijika kuona kuwa kuna mtanzania mwenzetu mwenye vipaji lukuki akiwa na itikadi ya kuondoa umaskini na kuleta ukombozi kupitia kazi zake hizo.
hongela mimi ni mmoja kati ya wasomaji wa nakala zako katika mwananchi
endeleza kutujuza tusio yajua
Nashukuru.
Ndugu Freddy,
Shikamoo, nakushukuru san kwa kuwa na moyo wa kujitolea katika kutujuza mambo mengi yanayotokea huku majuu. Mimi nilikuwa nafatilia sana makala zako kwenye gazeti la mwananchi tangu toleo la kwanza la “Kisa cha masudi” niliendelea kufuatilia pia na makala nyingine zinazohusiana na afya, mazoezi, matukio ya kihalifu yaliyokuwa yanajili huku UK hasa vijana kuchomana visu.
Kwa hakika, Makala zako zimenisaidia sana kuweza kuendana utamaduni tofauti na wa nyumbani. Nipo hapa Masomoni Marekani tangu Januari, 2010. Nimekuwa nikizirejea kumbukumbu za makala yako popote pale ninapotokewa na changamoto mpya hapa ugenini. Kusema kweli wewe ni zaidi ya Mwalimu, unatuelimisha kwa namna ya kipekee.
Kabla sijakwea pipa kuja huku, nilijaribu kuvitafuta vitabu vyako vya “Twen`Zetu Ulaya” na “Mpe Maneno Yake” kwenye maduka kadhaa huko Bongo yakiwemo, TPH,UDSM, na Furaha ilila sikufanikiwa kuvipata. brothe, Inakuwa vinakuwa adimu kiasi hicho? Pia nimejaribu kuvitafuta online stores such as Amazon and Ebay pia sijafanikiwa kuviona!
Kama una akiba hapo Nyumbani, nitumie kwa malipo.
Pia nilikuwa nashauri, uzichapishe zile makala za “kisa cha Masudi” kwenye mfumo wa kitabu ili iwe rahisi kuweka kumbukumbu za vizazi vijavyo na akina siye, si unajua jinsi gani ilivyo ngumu kuvikusanya vipande vya makala ya kila wiki kwa pamoja.
Keep it up! We are proud of you Brother.
Wazo la kuweka makala za nyuma katika mitandao mbalimbali, nimeshaanza kulifanyia kazi.
Ninakarabati tovuti yangu halafu ntaanza kuvipamba vitabu, blogu na mauzo ya CD na fasihi. Kwa sasa ukinitumia anuani yako Marekani naweza kukupostia kitabu cha Mpe Maneno Yake. Niandikie barua pepe tuwasiliane vizuri : kilimanjaro1967@hotmail.com
Thankz mr macha u made me understand before i go to abroad for ma degree studies thankz lot
Hey mr macha mm ni mgeni kabsa ktk nakala zako japo nshawah kukutana na kigazeti chenye title ya twendetu … Nilipenda falsafa za mwandishi na sikuwah kufatilia ila am anxious now to make follow up naomba web addres yako.
Tovuti yangu inakarabatiwa kwa sasa…. mtajulishwa baada ya muda…ahsante kwa kuulizia, Ggm.
Ila kama una haraka waweza tu kuni-google jina langu utakutana na mambo kibao.
hi bro am really apreciates ur article keep it up!
Kazi nzuri kila la kheri. Nategemea makala zijazo zitakuwa za kuvutia zaidi.
huyu ni genius hakuna kama yeye tena,anyoweza kupangilia mambo ni ajabu,,,,ana balaaa
Ni ukweli usiopingika Freddy unakonga… Endelea na Moyo huo huo
Ndugu Macha, mimi nilisoma Ilboru pia ila kwasasa nipo chuo kikuu Mzumbe ni mwandishi wa makala wa gazeti la Dira linatoka kila jumatatu pia ni blogger sasa naomba sana add blog yangu kwenye blog list yako….ni hayo tu kwa leo.
Ilinifurahisha Sana na nimekua mjuzi sasa.
Ola sinoir kitoto,Naitwa Burhan Ni Mkufunzi Wa kapoeira na nimeona umeshika berimbau hapo ikiwa kama kifaa kimojawapo cha muziki wa capoeira ningepenga tuwasiliane ili tupate xchage ideas na muziki maana kundi letu lipo ful jana tu tulikuwa na MEstra janja mwalimu wa kwanza kufudhu elime ya Kapoera daraja la umasta duniani na tumefanya workshop ya kutengeneza berimbau,kwa ufupi tuna berimbau aina zote medio,viola na gunga,tuna akabaki yani ngoma,recoreco,kengele za agogo, na pandeiro, tembelea https://www.facebook.com/groups/axedarcapoeira/, au blog yetu http://www.capoeira-in-dar.blogspot.com au tovuti yetu http://www.axxedarcapoeira.net76.net asante
Ahante Burhani…je wewe ni Mbongo au kabila gani? Ni vyema kujua kwamba Capoeira imeingia Tanzania. Nani aliileta?
Je, ni huyo Linda au nani? Mestre Janja ni nani? Samahani sikuona hii barua yako ningewatembelea nilipokua nyumbani karibuni.
Zamani nilikuwa nacheza Capoeira hasa nikiish Brazil. Siku hizi nautukuza tu muziki wake hasa wa Berimbau na Pandeiro.
Nadhani ni jambo zuri sana kwamba mchezo huu wa afya umeingia Afrika Mashariki hatimaye.
uko juu sana
Safi sana kaka na kazi nzuri….
Remarkable! Its truly awesome piece of writing, I have got much clear idea regarding from this piece of writing.
I have been exploring for a little bit for any high quality articles or weblog posts in this sort of space . Exploring in Yahoo I at last stumbled upon this website. Reading this info So i’m happy to exhibit that I have an incredibly excellent uncanny feeling I found out just what I needed. I so much undoubtedly will make certain to do not fail to remember this web site and provides it a glance regularly. As consequence: thank you and please please keep up the good work. I’ll surely come back and look for new stories! Best regards
Spot on with this write-up, I truly assume this website wants much more consideration. I’ll most likely be once more to read much more, thanks for that info.
I as well as my pals appeared to be reviewing the great hints found on your web page then suddenly I had an awful feeling I never expressed respect to the web blog owner for those secrets. Those young boys are actually so thrilled to learn all of them and have clearly been enjoying those things. We appreciate you getting considerably thoughtful and also for going for some fabulous information millions of individuals are really eager to be informed on. My personal honest apologies for not expressing appreciation to you sooner.
One thing I’ve noticed is the fact there are plenty of myths regarding the banks intentions while talking about foreclosed. One delusion in particular is the bank wishes to have your house. The lending company wants your hard earned money, not the house. They want the bucks they gave you having interest. Steering clear of the bank will simply draw any foreclosed final result. Thanks for your publication.
Thanks for sharing your ideas. The one thing is that students have a solution between fed student loan and also a private education loan where it can be easier to select student loan online debt consolidation than in the federal student loan./wp-login.php?action=registerOne thing is that when you find yourself searching for a education loan you may find that you will want a co-signer. There are many circumstances where this is correct because you might find that you do not use a past credit rating so the bank will require you have someone cosign the financing for you. Great post./wp-login.php?action=registerMany thanks for this article. I will also like to convey that it can end up being hard when you are in school and simply starting out to create a long credit rating. There are many pupils who are simply trying to pull through and have long or positive credit history can sometimes be a difficult matter to have./wp-login.php?action=registerI’ve learned quite a few important things via your post. I would also like to express that there might be situation where you will obtain a loan and never need a co-signer such as a Government Student Aid Loan. When you are getting a borrowing arrangement through a classic lender then you need to be made ready to have a co-signer ready to enable you to. The lenders will probably base their very own decision using a few aspects but the largest will be your credit history. There are some lenders that will also look at your job history and choose based on that but in many instances it will depend on your scores./wp-login.php?action=registerOne other issue is when you are in a situation where you don’t have a cosigner then you may genuinely wish to try to exhaust all of your money for college options. You will discover many funds and other scholarship grants that will ensure that you get funds to support with education expenses. Many thanks for the post.
I am not rattling good with English but I come up this very easygoing to understand.
Mfanyabiashara
first i wanna say thanks for let us know what is going on in uk but i want ask you would you help me to communicate with youth organization in uk .
Ungejiunga na Facebook na mashirika ya mawasiliano kama hayo. Haya mashirika ya vijana siku hizi ndivyo yanavyokwenda. Kutumia mitandao. Halafu kama wewe ukiwa mwanachama wa shirika la vijana hapo Bongo ni rahisi zaidi kujenga udugu na mashirika kama haya ugenini
Habari Kaka Macha?
Asante kwa habari zako nzuri na zenye maana, mvuto, utatuzi wa mambo mengi kwa jamii kwa ujumla, kuelimisha na kufurahisha sana. Nimekuwa nakusoma sana kwa gazeti la Mwananchi, ama kweli nakuombea sana kwa ALLAH, azidi kukutia nguvu na maono zaidi. Pia mara kwa mara, niingiapo humu kwenye blog yako, sichoki kupekua huku na kule. Pia kule kwenye wavuti yako, kwa kweli ni raha sana.
Kaka Macha, me ni kijana wa kitanzania. Ambaye napenda maendeleo halisia kwa jamii ya kitanzania. Nina ujuzi wa kujenga mitambo ya gesi ya asili, yaani (BIOGAS). Hivyo huwa nafurahi sana kuona nimefanikiwa kumwelewesha binadamu yeyote ambaye mfugaji umuhimu wa kujenga na kumiliki mtambo huo. Km ujuavyo kaka Macha, mazingira yetu yamekwisha kabisa kutokana na matumizi ya mwanadamu.
Kaka, ninachoweza sema hapa, ni kukupongeza kwa kila ukifanyacho kwa ajili ya jamii ya kitanzania, kiafrika na wenzetu popote hapa duniani. MWENYEZI MUNGU akuangazie zaidi kaka.
Nami napatikana kwa blog yangu ambayo ni http://www.biogastz.blogspot.com
naomba wadau wote waipitie kwa ufahamu zaidi wa teknolojia hii.
Rich.
Shukran Rich…tuko pamoja…
Habari za siku, hatimaye nimeweza kupata kitabu chako cha mpe maneno, kwani nilikitafuta sana , pia ninatafuata na kingine cha twede zetu ulaya, mimi ni mpenzi wa makala zako, ninakutakia kazi njema ya kuelimisha jamii.
Mpe Maneno Yake…ulikipata wapi? Kwani hakiko madukani siku hizi?
Twenzetu Ulaya tunajaribu kuangalia namna ya kukichapa tena ndiyo ahsante
naitwa joseph napenda kuwa mtangazaji na kuimba naomba kanuni za vipaji hivi
Kanuni za kazi zozote duniani ni wewe kupenda sana hiyo kazi, kupenda sana na kuwa na nidhamu nayo, si kufanya kwa ajili ya fedha au umaarufu; kuipenda. Halafu ukishapenda lazima ujifunze misingi yake. Kusoma na kujifunza ni kazi ya maisha yako yote. Kwa mfano nunua vitabu, nenda maktaba, tazama video, uliza waliobobea na kadhalika. Mwisho, usichoke aukukataa tamaa maana Mungu humsaidia yule anayejitahidi
Really informative blog post.Really looking forward to read more.
I’m extremely pleased to find this page. I need to to thank you for ones time just for this wonderful read!! I definitely appreciated every little bit of it and I have you saved as a favorite to see new things on your web site.
Hi brother F Macha!..nafurahishwa sana na makala zko za kalam kutoka london ila saa nyingine sizioni mtandaoni wakati ninapokua sehemu silipati gazeti la mwananchi jumapili.
Nashukuru…kaka.
Ni kweli si kila mara hawaweki Apolleo (mara nyingine kutokana na mitandao yetu Afrika Mashariki kutokua mizuri). Hivyo ningekuomba uwe unatembelea Blog langu liitwalo MAKALA ZANGU.
Nenda pale kupitia tovuti yangu : http://www.freddymacha.com/
Kisha bofya BLOGS.
Fredy hongera sana unafanya shughuli nzito kwa kweli.
I say congratulation brother.
naomba unijibu kupitia barua pepe
johndijacs@gmail.com
Kaka freddy shikamoo pole na majukumu. Pongezi kwako najifunza mengi katika makala zako. Zinanisaidia kutimiza ndoto zangu za kuwa mwandishi wa vitabu vya stori na sinema. Nimetafuta sana vitabu vyako maktaba nyingi hapa dar bila mafanikio vp nitavipataje?
Wachapishaji wangu wameniangusha miaka mingi. Lakini karibuni niko mbioni kurekebisha hali. Nashukuru kwa maoni yako
habari za london Fredy Macha
mie naitwa Dijacs John vilevile niko kuwa na blogu na andika habari ktk blogu.
hii ndiyo blog yangu
http://www.dijacse2.wordpress.com
mawasiliano na facebook
http://www.facebook.com/Dijacs
twitter @dijacs
simu yangu yangu ya mkononi +255789083203
mwanachuo kutoka mzumbe university.
asante sana kwa kushukuru unajua ulikuwa unazungumzia jambo la maana. kila la kheri london
kumbuka kutembelea blog yangu
http://www.dijacse2.wordpress.com
thanks a lot brother.
Macha napenda kazi zako fanya mpango nami nije huko ulaya. email me please dijacs@journalist.com
asante sana kaka mimeelimika vya kutosha Mungu akupe nguvu zaidi ili uendelee kutupa vitu vya nguvu
Mie mamamkubwa na kwa jina rasmi ni Adeline Gara , Mtanzania halisi umri yapata miaka 56 sasa. Nimependezewa na habari zako kijana Freddy.
Katika kila jamii duniani kuna desturi zafaa kuigwa na kuendelezwa.
Najivunia uafrika na kukaa natural kwa ngozi na nwele pilipili kama nilivyoumbwa.
Nawashauri wanawake wa Kiafrika kuwa hata nywele na ngozi yetu wazungu wanazitamani. Tumaintain maana twapendeza
Adeline – nashukuru kwa maoni yako. Nashukuru kwa wewe kutukuza Uafrika na uzuri asilia. Pia nakupa ahsante kwa kuniita kijana ….hata kama nimekuzidi sana umri!
Hello Frady how can I get your mobile pls call us
My name is Daniel
What’s app +1 904 717 2394
Mobile +255 657 598 386