Mwezi Septemba 2001, ulimwengu ulikuwa na utata na mashaka baada ya tukio la ugaidi New York. Siku moja nyakati hizo nikakaa na mwanamuziki na “projuza” kijana, Gabriel Prokofiev, rafiki wa miaka mingi tukasema kwanini tusitoe kibao cha furaha kufuta machozi?
Moja ya nyimbo nilizotunga nikiishi Brazil (1989) ni wasifu wa mlima Kilimanjaro : asili, fahari na sura ya Waafrika. Unafahamika kwa jina ila wengi hawafahamu ulipo… hudhani ni Kenya. Ah basi, mwezi wa Oktoba 2001, tukakusanyana wanamuziki mbalimbali toka Ulaya, Afrika Mashariki na Kati. Mkusanyiko ukatimia studio- chini ya fundi mitambo Gabriel Prokofiev.
(more…)