Nilizaliwa Kilimanjaro na kusoma Tela, Natiro kisha Kaloleni na Ilboru mjini Arusha. Baada ya kumaliza kidato cha sita Mzumbe nilijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa, Mafinga, Iringa na kuanza kazi ya uandishi wa habari magazeti ya Kiswahili; Uhuru na Mzalendo, mwaka 1976. Kuanzia hapo nimekuwa mwandishi wa habari, magazeti, redio, muziki, sinema na sanaa za maonyesho. Nilikuwa mwanasafu wa Sunday News, kila Jumapili, kwa Kiingereza (Cultural Images) hadi mwaka 1984. Nimeshachapa vitabu kadhaa: Twenzetu Ulaya (84), Mwanamuziki Remi (86), Papers! (1986) na Mpe Maneno Yake (2006). Nishatoa albam kadhaa ila inayojulikana zaidi ni Constipation (2000). Nishazunguka sana duniani, nikasoma na kuishi Brazili miaka Saba na nchi nyingine kama Kanada, Paraguay, Kenya nk, kwa sasa naishi London nikiandika, nikifundisha, nikifanya kazi za ukalimani, michezo na kupiga muziki na bendi yangu, Kitoto.