Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘Kujitegemea’

Mganga na mtaalamu wa maradhi ya moyo katika hospitali ya Guy’s and St Thomas, mjini London kakumbusha kwamba unene ni moja ya asili ya vifo duniani. Kashauri  mbali na kula na mazoezi wewe mwenyewe unaweza kutazama kama u hatarini kwa kujipima kiuno.

Daktari Graham Jackson anasema chukua  rula ya mshipi (inayotumiwa na washoni) iweke sentimeta moja au mbili juu au chini ya kitovu. Zungusha nyongani. Kiuoni kikizidi sentimeta 100 (inchi 39) kwa wanaume na sentimeta 85 (inchi 33) kwa wanawake basi una hatari ya kupata kisukari na magonjwa mengine ya unene mathalan: kiharusi, hinikizo nk.

Read Full Post »

Mwanablogu Maggid akipozi na F Macha baada ya kuhudhuria semina ya Nyumba Ya Sanaa

Mjadala aliopopoa Maggid ” Mwenyekiti”  Mjengwa (pichani, kulia, alipohudhuria semina zangu,  Dar, Mei)  blogu ya Kwanza Jamii umezua maoni kem kem.  Ni mjadala muhimu kwa sababu kadhaa:

1-Zamani Mwalimu Nyerere alisisitiza sana juu ya utaifa ndiyo maana akashauri sote tuongee Kiswahili. Hii imechangia sana kutokuwa na kero za ukabila Tanzania kama zilivyo nchi nyingi bara Afrika. Hatujawa na vita vikubwa vya wenyewe (ukiacha kumtoa Amin, 1979) tangia 1907.

2-Kizazi kipya cha Watanzania kilichopumua hewa baada ya  Mwalimu  (Ujamaa) kimeanza “kukua na utata” wa kutojijua wewe nani (identity) hili linaonekana mathalan katika masuala ya lugha.  Lugha ni kitanda kikuu cha mawasiliano na utamaduni. Wachache sana leo wanaweza kuandika au kuongea Kiswahili fasaha au Kiingereza fasaha bila kuchanganya maneno.  Tatizo hili limeenea Afrika nzima. Wazaire,  kwa mfano wakiimba au kuongea utakuta sentensi zimechanganya Kilingala na Kifaransa. Wakenya hivyo hivyo. Afrika Kusini hivyo hivyo.

3-Hata wale wanaondika Kiswahili utakuta wanachanganya herufi L na R  ama  DH na Z .

Mathalan : “luka” badala ya “ruka”;  “luninga” kinyume cha “runinga”; “azabu” badala ya “adhabu” nk. Hili ni tatizo kubwa sana na linaonekana wazi wazi  ndani ya mablogu, vyombo vya habari, simu za mkono (SmS) , nk.

4-Mfano bab kubwa wa karibuni ni malumbano na mgogoro kuhusu mwigizaji  Steven Kanumba, alipokuwa katika Big Brother Afrika, anadaiwa na baadhi eti hakuongea Kiingereza fasaha (ingawa suala ni la lafudhi na nahau kuliko sarufi) na  alikosea alipotoa zawadi ya shati rangi ya waridi – pink- (ambayo ni rangi ya Wasenge ughaibuni) badala ya kutoa kitu cha jadi kama vinyago,  kanga, miziki ya Watanzania nk.

Mambo kama haya ya utoaji zawadi kutoka kwenu….(mila na desturi) hutokana na kujijua yaani “identity” anayoongelea Mwenyekiti Maggid.

Hebu angalia maoni chini:

http://mjengwa.blogspot.com/2009/09/watanzania-hatuna-kwetu.html#comments

Read Full Post »