Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘Adam Shafi’

MbalinaNyumbani-jalada SHAFI
Juma hili habari kwamba kitabu kipya cha mwandishi nguli, Adam Shafi (Kasr ya Mwinyi Fuad,Kuli, Vuta Nkuvute na Haini) kimetoka ni za kushangilia sana. “Mbali na Nyumbani” inaangalia maisha yake msanii huyu Ughaibuni takribani miaka 50 iliyopita…Kimetolewa na Longhorn Publishers wenye makao yao Nairobi Kenya na matawi mbalimbali Dar es Salaam, Kampala na Rwanda.
Mara ya mwisho nilipomhoji Mzee Shafi, Desemba 2007 alikuwa bado anakiandika kitabu hicho ambacho alisema kitaelezea maisha yake ya ujanani.
shafi na MJUKUU LOWELL
Shafi akiwa na mjukuu wake Lowell, mjini Milton Keynes, Uingereza. Picha na F Macha

Katika uchambuzi wa kitabu hicho, mwandishi hodari wa Kenya, Profesa Ken Walibora, anasema mtindo wake wa kuangalia tawasifu- ambapo mwandishi au mhusika anaelezea maisha yake haujaenea sana katika maandishi ya Kiswahili seuze ya Kiafrika. HIvyo anasema Walibora, ni jambo zuri la sisi wengine pia kulifanya.
Mbali na kutukuza kitabu hiki, Profesa Walibora anachangamkia namna maandishi na lugha ya Kiswahili inavyoendelea kukua duniani. Hivyo kututaka Waswahili kuendelea kuandika na kujenga na kuimarisha KISWAHILI.
MUSWAADA WA KITABU CHA SHAFI
Mwanafasihi Shafi akinionyesha muswaada wa kitabu hicho -wakati kikiwa bado jikoni miaka mitano iliyopita.
Ni jambo la kuchangamkia kwamba kimemalizika. Picha na F Macha.

IMG_3066[1]
Kuli, kilichotolewa mwaka 1979 (TPH) na 2005 na Longhorn, ni moja ya vitabu maarufu vya mwandishi ambavyo vimempatia sifa ya kuiangalia jamii yake kwa macho ya darubini kali ya kimaendeleo.

Shafi- Kasr ya Mwinyi Fuad
Kasr ya Mwinyi Fuad, toleo lake la kwanza kabisa, lilitolewa pia na TPH mwaka 1978. Kitabu hiki kimeshatafsiriwa katika Kifaransa, jambo linaloonyesha namna mwandishi huyu anavyosifika duniani.

SOMA TAHAKIKI YA PROFESA KEN WALIBORA (aliyehariri na kuchangia kitabu kizuri sana cha Kiswahili, pamoja na Profesa Said Ahmed Mohammed, DAMU NYEUSI, kilichotolewa na MacMillan Kenya, 2007!)
http://www.swahilihub.com/habari/MAKALA/-/1310220/1672466/-/ouhmen/-/index.html

Read Full Post »

adam-shafi.jpg

Nimepokea simu. Simu ya maana. Adam Shafi yuko Majuu. Kaja kikazi Uholanzi. Yeye mtaalamu wa lugha ya Kiswahili. Baada ya kumaliza kapitia Uingereza katika mji mmoja wenye wakazi wengi wa Kitanzania, yaani Milton Keynes. Ni wastani wa saa moja kwa treni toka London.  Mrefu, mchangamfu, mzungumzaji aliyesheheni “mastore” kibao. Nishakutana na waandishi wa kila sampuli. Wanaojificha: wakimya, wasioongea sana, wapole wanaokaa chumbani kati kati ya watu ukadhani hawapo. Wanaopiga kelele, wakijafaragua; ama wenye aibu…
Shafi ni mtu wa kawaida kabisa, naweza kuiita hulka, tabia na namna yake “Mfurahia Maisha” : kachangamkia  uhai, haswa. Kaishi, anaishi…hamalizi. Kila mara atasema ana mikakati ya kufanya jambo fulani, kuandika kitabu kingine kipya, kuendeleza fasihi na Kiswahili….
(more…)

Read Full Post »