Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘Zanzibar’

https://youtu.be/jjk8Nca9sPQ

Picha na Habari za Freddy Macha

Wangapi tumewahi kusikia mashindano ya kimataifa ya mashua za upepo (“clipper race” )? Mimi sikuyajua hadi nilipomhoji Nassoro Mahruki, Mzanzibari mshiriki wa tukio hilo litakalochukua miezi kumi na moja hadi Agosti 2020.
Nassoro Mahruki ambaye huendesha shughuli zake za biashara za utalii visiwani Pemba na Unguja, ni Mwafrika Mashariki pekee na anasema alijitayarisha kwa miaka miwili kushiriki.
“Yakubidi ufanye mafunzo na kufaulu …” alisema akinionyesha mashua iitwayo “Zhuhai” ikiongozwa na nahodha Nick Leggatt. Zhuhai ni kati ya vyombo vingine kumi na moja vyenye majina kama “Korea”, “Punta Del Este”, “WTC Logistics”, nk.
(more…)

Read Full Post »

Riwaya zako tatu zimepishana miaka 36. Je kwanini, muda mrefu toka Utengano hadi Nyuso? Asali Chungu (1977), Utengano(1980) na Nyuso za Mwanamke (2010), Mhanga Nafsi Yangu (2012).
Vile vile dhamira kuu inamwangalia mwanamke kwa macho na hisia za kumtetea. Mwandishi mwingine Mwafrika anayesimama upande wa kina mama (hasa vitabu vyake vya mwanzo) ni Msomali – Nuruddin Farah. Je, kwanini wanaume muwatetee wanawake? Kwani hawawezi kuandika wenyewe?

Nyuso za Mwanamke
Mwandishi Said Ahmed Mohammmed
Kuandika riwaya au kazi yoyote ya fasihi kunahitaji wakati, utulivu na wiitisho wa ndani wa nafsi ya mwandishi. Huwezi tu kujilazimisha kufululiza. Kisha nadhani vita vya wanawake ni vita vya wanaume pia kama ilivyo kwamba vita vya wanaume ni vita vya wanawake. Kwa hali hii hakuna suala la kwa nini? Kwa bahati mbaya waandishi wanaume wachache tu ndio wenye msimamo wa ukombozi wa wanawake katika fasihi ya Kiswahili. Ama suala la wanawake kutoandika wenyewe wapo wachache katika fasihi ya Kiswahili wanaoandika hata kwamba hawajitetei. Jambo hili linashikamana na historia ya wanawake katika jamii zetu. Wanawake popote pale wamekuwa katika historia ya ukandamizwaji, je kwa nini tusiwatetee?.
(more…)

Read Full Post »

Prof Said Ahmed Mohammed
SEHEMU YA KWANZA ya mahojiano kati ya Freddy Macha na Profesa Said Ahmed Mohammed mwandishi wa zaidi ya vitabu 30 vya Kiswahili.
Profesa Said, umeandika vitabu vingi. Ama kweli wewe ni hazina ya fasihi ya Kiswahili ambaye hujapata heshima inayokustahili. Najua hupendi kusifiwa – lakini lazima tukuthamini ungali hai maana wewe fahari yetu Waswahili. Hata ukiweka neno “Tanzanian Novelists”, “Zanzibar Writers”, au “Tanzanian Writers” katika Wikipedia hutajwi. Unadhani kwanini wengi hasa Tanzania bara na visiwani hawakufahamu ipasavyo?

Mwandishi : Said A Mohammed
Kama nilivyokueleza katika mkumbo wa masuali uliyoniuliza mwanzo hapo kitambo, Watanzania na zaidi Wazanzibari hawana utamaduni wa kusoma vitabu vya fasihi. Kwa hivyo hawajapata ari wala mwamko wa kujali na kuthamini fasihi yenyewe na waandishi wake. Kweli kuna wachache ambao wanatangazwa katika vyombo vya mawasiliano, lakini mimi simo katika orodha ya waandishi hao. Hili ni suala la vyombo vya habari ambavyo mara nyingi huwatukuza wale ambao wanataka wao watukuzwe. Vilevile kuna wasanii wanaopenda kujipeleka mbele ili wasikike na hata kuwa na fikra kwamba waandishi wengine wadidimie. Kwa bahati mbaya au labda kwa bahati nzuri, mimi si mtu wa kimbele mbele. Naamini sana maneno ya wahenga kwamba Kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza.
Asali Chungu
Katika dunia ya sasa kujipeleka mbele ili usikike bila umakinifu, ndilo jambo linaloharibu mambo mengi ikiwemo sanaa ya lugha. Vipawa vinadharauliwa na sanaa tunazokutana nazo ni sanaa zinazokuzwa tu bila ya kupitiwa kwa kina na kujadiliwa. Chambilecho, gwiji wetu wa fasihi, Profesa Ebrahim Hussein, hakuna fasihi tena kwa maana ya fasihi. Hakuna wasomaji wazingatifu. Hakuna uhakiki kwa maana ya uhakiki. Kuna fikra ya kwamba chochote kile ni sawa. Shairi, riwaya, hadithi fupi au tamthilia ikiwa ina sura ya tanzu inayohusika, basi ni fasihi tu kwa maoni ya wengi. Fasihi haipo. Wasomaji hawapo. Umakinifu wa fasihi haupo. Uhakiki umepotea. Hata wale ambao tunawatarajia kufanya hivyo hawashughuliki na kusoma, kuandika, kuhakiki na kuzitangaza kazi za fasihi ya Kiswahili. Sisi waandishi hatuwezi kujitetea. Wanaojitetea na kuwaponda wenzao ndio katika hao wanaowekwa mstari wa mbele na wanaojitapa kuwa wanajua hata kuandika kazi za waandishi wenzi wao.
Mashairi Watoto-Said A Mohammed
(more…)

Read Full Post »

MbalinaNyumbani-jalada SHAFI
Juma hili habari kwamba kitabu kipya cha mwandishi nguli, Adam Shafi (Kasr ya Mwinyi Fuad,Kuli, Vuta Nkuvute na Haini) kimetoka ni za kushangilia sana. “Mbali na Nyumbani” inaangalia maisha yake msanii huyu Ughaibuni takribani miaka 50 iliyopita…Kimetolewa na Longhorn Publishers wenye makao yao Nairobi Kenya na matawi mbalimbali Dar es Salaam, Kampala na Rwanda.
Mara ya mwisho nilipomhoji Mzee Shafi, Desemba 2007 alikuwa bado anakiandika kitabu hicho ambacho alisema kitaelezea maisha yake ya ujanani.
shafi na MJUKUU LOWELL
Shafi akiwa na mjukuu wake Lowell, mjini Milton Keynes, Uingereza. Picha na F Macha

Katika uchambuzi wa kitabu hicho, mwandishi hodari wa Kenya, Profesa Ken Walibora, anasema mtindo wake wa kuangalia tawasifu- ambapo mwandishi au mhusika anaelezea maisha yake haujaenea sana katika maandishi ya Kiswahili seuze ya Kiafrika. HIvyo anasema Walibora, ni jambo zuri la sisi wengine pia kulifanya.
Mbali na kutukuza kitabu hiki, Profesa Walibora anachangamkia namna maandishi na lugha ya Kiswahili inavyoendelea kukua duniani. Hivyo kututaka Waswahili kuendelea kuandika na kujenga na kuimarisha KISWAHILI.
MUSWAADA WA KITABU CHA SHAFI
Mwanafasihi Shafi akinionyesha muswaada wa kitabu hicho -wakati kikiwa bado jikoni miaka mitano iliyopita.
Ni jambo la kuchangamkia kwamba kimemalizika. Picha na F Macha.

IMG_3066[1]
Kuli, kilichotolewa mwaka 1979 (TPH) na 2005 na Longhorn, ni moja ya vitabu maarufu vya mwandishi ambavyo vimempatia sifa ya kuiangalia jamii yake kwa macho ya darubini kali ya kimaendeleo.

Shafi- Kasr ya Mwinyi Fuad
Kasr ya Mwinyi Fuad, toleo lake la kwanza kabisa, lilitolewa pia na TPH mwaka 1978. Kitabu hiki kimeshatafsiriwa katika Kifaransa, jambo linaloonyesha namna mwandishi huyu anavyosifika duniani.

SOMA TAHAKIKI YA PROFESA KEN WALIBORA (aliyehariri na kuchangia kitabu kizuri sana cha Kiswahili, pamoja na Profesa Said Ahmed Mohammed, DAMU NYEUSI, kilichotolewa na MacMillan Kenya, 2007!)
http://www.swahilihub.com/habari/MAKALA/-/1310220/1672466/-/ouhmen/-/index.html

Read Full Post »

Mahojiano na mtaalamu, mtafiti na mwandishi wa Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru!  Zanzibar na Mapinduzi ya Afrabia

Dk. Harith Ghassany ni mwandishi wa kitabu kinachoongelewa Tanzania nzima sasa hivi na huenda kikavuka mipaka na kuingia nchi nane zinazopakana na Jamhuri ya Muungano. Kitabu hiki chenye kurasa 500, kinazungumzia namna gani Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 yalipikwa Dar es Salaam, Algeria  na mashamba ya mkonge ya Tanga na kupakuliwa Zanzibar. (more…)

Read Full Post »

Jamii zetu zinazoendelea zinahitaji sana Elimu.  Elimu itakayotusaidia kupambana na maadui kama : kutojua kupanga muda (Time Management) tatizo linalotufanya tuchelewe, tusiwe na mpangilio wa maisha ; halafu, kutoyajali mazingira yetu (vyoo vichafu na kutupa taka ovyo).Uchafu wa mazingira DarWataalamu wameshatuonya kuwa makaratasi ya plastiki tunayoyaacha kiholela kila mahali (yenye madawa hatari) yanaharibu rutuba na uhai ; yatakaa ardhini miaka 500 !!!

Bougainvillea -Silversands

Si mbali  na palipotupwa plastiki hizi pana hoteli hii marufu na nzuri ya Silversands ambapo watalii na wenye uwezo wanakaribishwa kwa maua  mazuri yenye asili ya Kimarekani yaitwayo Bougainvillea.  Ikiwa tunaweza kuyapamba mazingira ki-azizi,  hatushindwi kuyaacha safi…

Madafu

Nilishangazwa nilipoelezwa na muuza madafu mmoja Dar kuwa kinywaji (chakula) hicho muhimu siku hizi hakipatikani kirahisi. “Minazi inakatwa ovyo…” akalalama. 

Minazi ya Dole

Nilipokuwa kitongoji hiki cha Dole, Unguja, nikawa nawaza lile balaa la minazi kukatwa bandari  ya Dari Salama. Minazi imesimama dede mithili ya twiga au mbuni malishoni.  Je, itadumu? 

Matunda ya Afrika  Sehemu nyingi Zanzibar bado vyakula asilia vinathaminiwa. Cheki  matunda, mboga na makulaji : mjini na vijijini. Ama kweli inatia moyo…maana chakula ni utamaduni wa nchi; kama huna au unaiga (huthamini chako) huna jicho…

Chakula cha Zanzibar

Huku unakula huku unafikiria namna ambavyo bado wananchi wengi tunatupa chupa za maji ovyo nje; tunavyofungia bado vyakula vyetu kwa magazeti badala ya mifuko isiyokuwa na sumu na madawa… 

Chupa ya maji- uchafu

Kinamasi hiki kimejaza si tu plastiki  na dawa zenye sumu bali pia wadudu kama mbu. Kila anayeweza (kutumia mtandao na kompyuta ni uwezo na nafasi) kuelemisha watu wetu ajitahidi na kujaribu…maana hizi blogu hazisomwi na wengi.

Silversands-2

Hapa natia tizi katika moja ya bichi za Dar…ukweli si rahisi siku hizi kupata ufukwe msafi mjini hapa. Na hata zile safi baada ya kuogelea unahisi macho yakikuwasha washa. Watalaam wameonya kuhusu kutupa taka ovyo baharini, kunya (na kukojoa) ovyo ufukweni, kuchafua michanga kwa vyupa vya vinywaji tunapostarehe kando ya bahari mama ya Hindi.

Jani la Mnazi

Pwani ya Dar

Read Full Post »

adam-shafi.jpg

Nimepokea simu. Simu ya maana. Adam Shafi yuko Majuu. Kaja kikazi Uholanzi. Yeye mtaalamu wa lugha ya Kiswahili. Baada ya kumaliza kapitia Uingereza katika mji mmoja wenye wakazi wengi wa Kitanzania, yaani Milton Keynes. Ni wastani wa saa moja kwa treni toka London.  Mrefu, mchangamfu, mzungumzaji aliyesheheni “mastore” kibao. Nishakutana na waandishi wa kila sampuli. Wanaojificha: wakimya, wasioongea sana, wapole wanaokaa chumbani kati kati ya watu ukadhani hawapo. Wanaopiga kelele, wakijafaragua; ama wenye aibu…
Shafi ni mtu wa kawaida kabisa, naweza kuiita hulka, tabia na namna yake “Mfurahia Maisha” : kachangamkia  uhai, haswa. Kaishi, anaishi…hamalizi. Kila mara atasema ana mikakati ya kufanya jambo fulani, kuandika kitabu kingine kipya, kuendeleza fasihi na Kiswahili….
(more…)

Read Full Post »