Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘SAGCOT’

WAZIRI NA WENZAKE WASISITIZA HAJA YA WALOWEZI KUCHANGIA MAENDELEO BONGO
Imeandaliwa kwa ushirikiano wa Urban Pulse na Freddy Macha

Watanzania waliokuwepo wakichangamkia maongezi

Watanzania wakazi Uingereza wamehakikishiwa kuwa taaluma na uzoefu wao ughaibuni vitasaidiwa na vyombo husika vya serikali wakirejea na zana, mbinu na uwekezaji wa kilimo.
Kauli hii ilitolewa na msafara mzima wa viongozi uliofuatana na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi Christopher Chiza alipokutana na Watanzania Ubalozini, London , Jumatano iliyopita.
Mininster Eng Chiza speaks at TZ Embassy UK-pic by Urban Pulse
Waziri Chiza alisema akiwa mtoto wali uliliwa siku za sikukuu tu. Leo mengine. Mchele unapandwa zaidi na bado hautoshi.

(more…)

Read Full Post »

Imeandaliwa kwa ushirikiano wa Urban Pulse na Freddy Macha

MP Henry Bellingham chairs meeting-pic by Urban Pulse

Wawekezaji wamehimizwa kutosikiliza propaganda za uongo kuhusu uporaji ardhi Tanzania na kuendeleza miradi ya kilimo nchini.
Akiongea katika mkutano wa wafanyabiashara na viongozi wa taasisi, mashirika na makampuni mbalimbali ya ukulima na mazao Uingereza na Tanzania, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi Christopher Chiza alisisitiza serikali iko tayari kumsaidia yeyote anayetaka kuchangia idara hii muhimu ya uchumi.
Waziri  Chiza akihutubia ukumbi wa Reform Club London-pic by Urban Pulse
Waziri akihutubia…

Waziri Chiza aliyewasili London Jumatatu, kwa ziara ya kiserikali ya siku tano akiongoza msafara wa wanataaluma wa kilimo, alikuwa akijibu swali lililoulizwa mara kadhaa kuhusu ugawaji ardhi Tanzania.
Alifafanua: “ Lipo gazeti moja lilisema serikali imechukua hekta milioni tatu. Si kweli. Ardhi iliyoshakaguliwa katika miaka miwili iliyopita si zaidi ya hekta 4,000. Habari hizi zimesababisha Tanzania kuondolewa katika kundi la nchi za kuwekeza kilimo. Hata wafanyakazi wa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanatangaza uongo huu ambao ni marudio tu ya mambo yasiyo kweli yaliyoshazushwa zamani. Tafadhali njooni muongee na sisi wizarani na serikalini au taasisi zinazoaminika kama SAGCOT. Tutawaambia ukweli na kufanya nanyi kazi.”
(more…)

Read Full Post »