Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘Utenzi’

1- Fab Moses akiitongoa shairi lake- Pic by F Macha.jpg

Hakuna aliyetegemea.

Kila mhusika pale alikuwa akimsalimia  Makamu wa rais, Mheshimiwa Samia Suluhu na wageni wengine. Ilipofika zamu yake mwanamuziki Fab Moses, hisia zilimkwea ghafla kama utiriri. Ingawa ki- itifaki haikupangwa, maneno na ari ya utenzi ule wa Kiswahili, (mbele ya wadau wa mataifa mbalimbali), yalichangamshaa na kupigiwa makofi na vigelegele.

Fab Moses ni msanii mwenye vipaji kadhaa ikiwemo uchezaji sarakasi, uimbaji wa nyimbo za Kiswahili,  utunzi wa muziki , tenzi, nk.

Sasa hivi ni pia mwenyekiti wa Wasanii Tanzania Uingereza (WASATU) inayotazamiwa kuendesha sherehe rasmi, ukumbi wa Heartlands, Birmingham Jumamosi ijayo, tarehe 28 April kuanzia saa moja jioni hadi tisa usiku.

Fuatilia habari zaidi Instagram

Alama Reli WASATU.

3-bango la WASATU.jpg

 

Read Full Post »