Vielelezo vya kitabu cha hadithi za Daudi vilivyosanifiwa na Raza kufundishia Kiingereza mashuleni Bongo, miaka ya 80…
Mchoraji, msanii, mpambaji wa taswira, vitabu na stempu, Raza Mohamed anatazamiwa kufanya maonyesho ya picha zake katika ukumbi wa Mulberry Tea Room, Charlton House, kitongoji cha Greenwich, London, Ijumaa tarehe 17 Juni hadi Jumatano 20, Julai mwaka huu.
Msosi wa Biriani, kachumbari, pilipili, nyama kwa nazi aliopika binti yake Raza kutukaribisha wakati wa mahojiano jana. Ama kweli kila jambo katika ukoo huu lina tone na wajihi sanifu…
Charlton House ni kasri kubwa la kale lililojengwa karne ya 17 enzi za utawala wa mfalme James wa Kwanza. Lina miti, bustani kubwa maridadi, maktaba, maonyesho ya muziki, vyumba vya masomo mbalimbali, vyumba vya mikutano na mgahawa. Ni jengo linalotukuza utamaduni, elimu, burudani, historia na mila ya Waingereza na wageni wao, hasa wakazi wa Greenwich.
Charlton House
Kifupi, ni mahali pa hadhi. Raza na mwanae kukubaliwa kuonyesha kazi zao hapa ni heshima kubwa kwa jina la Watanzania wote. Ni mabalozi wanaowakilisha taifa kwa sanaa yao ya picha tupu.
Raza na picha ya “Watoto wakicheza Mdaku” iliyopikwa Unguja. Picha na F Macha.
Raza Mohamed ambaye ni hazina ya taifa letu amekuwa akichora toka akiwa mtoto wa miaka sita tu mwaka 1952. “Nilianza kwa mkaa…” alisema nilipomhoji nyumbani kwa mwanae, jana. (more…)
Read Full Post »