Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘Saidi Kanda’

PICHA NA HABARI 

Za Freddy Macha

3-bango la WASATU

Jumuiya ya Wasanii Watanzania Uingereza (WASATU)  ilichemsha supu, ukumbi wa Heartlands , Birmingham, Uingereza Jumamosi iliyopita. Makutano haya yalikuwa pia sehemu ya mchango mahususi kusaidia wasichana wanaopewa mimba kabla ya kuwa watu wazima, vijijini,  Arusha. Fedha zilikusanywa na mjasiria mali mkazi wa Birmingham, Mtanzania Sia Travel. Sia alijaa mlangoni akihakikisha kila senti iiliyolipwa na wahudhuriaji watashiba chakula ,  sanaa  usiku kucha na kuwafariji vigoli wetu, Tengeru.
(more…)

Read Full Post »

fab-moses-a-r-migiro-na-saidi-kanda-pic-by-f-macha-2016

Mcheza  Sarakasi na mwanamuziki Fab Moses na mwenzake mwana muziki nguli Saidi Kanda wakiwa na Mheshimiwa Balozi, Asha Rose Migiro baada ya kikao cha Jumatano iliyopita London.

Wasanii wanane waligonga milango ya Bond Street. Ikafunguliwa. Wakakaribishwa. Msaidizi wake mheshimiwa akawataka kukaa. Kaeni. Bw Allen Kuzilwa huyo.. Juu  ghorofa ya kwanza. (more…)

Read Full Post »

This slideshow requires JavaScript.

Maadhimisho ya miaka 40 ya urafiki kati ya Uingereza na Tanzania (BTS) yalifanyika mjini Reading, Jumapili 8 Novemba 2015. Wanamuziki watatu wa Kitanzania walialikwa kutumbuiza kwa mseto wa midundo ya kijadi na kisasa : Chakacha, Ilimba, Rumba na ngoma maarufu ya mkoa wa pwani iitwayo BUTI.
(more…)

Read Full Post »

Kitoto ni ngoma ya Kusini, Tanzania. Kitoto kwangu ni mashangilizi ya ngoma na utamaduni wa Mwafrika.
Hizi ni baadhi ya shughuli ambazo mwana Kitoto hufanya ughaibuni. Usiku na mchana. Ninazionea fahari…

Miaka mingi wengi wameniuliza watakujaje Majuu. Njia nzuri na rahisi sana ni kufanya mambo ya kwetu. Ngoma ni kitu kinachopendwa na wageni maana ni uhalisia na asili ya Mwafrika.

Juu hapa wanaonekana wanamuziki wawili wa Kitanzania wanaoishi Uingereza. Saidi Kanda na Fab Moses. Fab Moses hucheza sarakasi, huimba na kucheza ngoma. Mpiga ngoma maarufu aliyekuwa zamani na Remmy Ongala, Saidi Kanda kashika marimba. Marimba ya Kitanzania ndiyo. Vitu vyetu hivyo.

Kitoto tunapiga mashairi, ngoma na kuicheza. Hapa ni usiku wa kusaidia fedha za kupunguza ukeketaji Tanzania, London, 2014. Ngoma oyee!

(more…)

Read Full Post »