Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘KIswahili culture’

PICHA NA HABARI 

Za Freddy Macha

3-bango la WASATU

Jumuiya ya Wasanii Watanzania Uingereza (WASATU)  ilichemsha supu, ukumbi wa Heartlands , Birmingham, Uingereza Jumamosi iliyopita. Makutano haya yalikuwa pia sehemu ya mchango mahususi kusaidia wasichana wanaopewa mimba kabla ya kuwa watu wazima, vijijini,  Arusha. Fedha zilikusanywa na mjasiria mali mkazi wa Birmingham, Mtanzania Sia Travel. Sia alijaa mlangoni akihakikisha kila senti iiliyolipwa na wahudhuriaji watashiba chakula ,  sanaa  usiku kucha na kuwafariji vigoli wetu, Tengeru.
(more…)

Read Full Post »

Flyer by Evelina Moceviciute 2015
Mwanamuziki mkazi London, Freddy Macha, anatazamiwa kutumbuiza kwa ngoma na muziki wa gitaa, kwenye tafrija ndogo kutangaza na kuuza picha za watoto wa Kitanzania. Tafrija na maonesho yametayarishwa na wapiga picha watatu wa Kizungu, Amy Read, Evelina Moceviciute na Saraya Cortaville waliofanya kazi za kujitolea Mbeya vijijini mapema mwaka huu. Mauzo ya taswira yatatumika kusaidia maisha na elimu ya watoto hao hao waliopigwa picha. Mradi mzima unaitwa “Ahsante Children”…kutukuza na kutangaza lugha ya Kiswahili, Tanzania na wananchi Afrika Mashariki.
Onesho litafanywa mkahawa wa
The Chapel
St Margaret’s House,
21 Old Ford House,
Bethnal Green,
Hackney, London E2 9PL.
Jumapili 4 Oktoba 2015.
Saa 11 na nusu jioni hadi 3 usiku.

HABARI ZAIDI
http://www.freddymacha.com/
Freddy Drums - Germany May 2012- pic by Luis Tome Passarello
Freddy Macha na ngoma. Picha ya Luis Tome Passarello

Read Full Post »

TAREHE 29 OKTOBA, 2010….

Kuunganisha  chuo cha  SOAS na jumuiya ya Wazungumzaji  KISWAHILI Uingereza…

‘Milima haikutani, bali wanadamu hukutana’

Sherehe itafanywa  wapi?

Chumba cha  G50,   SOAS, Russell Square,

Thornhaugh Str.

London WC1H OXG

Saa moja jioni – MBili na nusu usiku. Kiingilio BURE. Karibuni

FAROUK TOPAN, mhadhiri wa KIswahili atafungua dimba la  SWAHILI SOCIETY. Uzinduzi utatangaza rasmi tovuti ya Kiswahili:

www.swahilisociety.com

SHEIKH MBARAK  ataongelea kuhusu ” Maisha ya Kiswahili  Nje ya Afrika, mjini London.”

FREDDY MACHA atawasilisha mada kuhusu ‘ Mzizimo wa Jumuiya ya Kiswahili Mtandaoni”‘

SOKO,  wauzaji wa mavazi ya Kitanzania , wataonyesha walicho nacho.

Mgawaha wa  KILIMANJARO utauza Chakula cha  Kiswahili

Mwishowe bendi ya  KITOTO,  itatumbuiza   ukumbi wa JCR  kuanzia saa tatu usiku.

Mtangazaji na mwanahabari, Ayoub Mzee  toka Swahili Diaries SKY news, atawakilisha habari hizi!

KARIBUNI!!!

Habari zaidi ongea na Jason Tuff  (pichani chini) akiwa Mdawi, Kilimanjaro, alikokuwa akifanya mazoezi ya Kiswahili…


Jason ni mmoja wa Waingereza wanaopigania hadhi ya Kiswahili nje ya Bongo na mchangiaji wa klabu hii mpya ya Waswahili SOAS.

Simu…. +44-7816-642296

Barua pepe : 212894@soas.ac.uk

Read Full Post »