Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘RamaSax’

PICHA NA HABARI 

Za Freddy Macha

3-bango la WASATU

Jumuiya ya Wasanii Watanzania Uingereza (WASATU)  ilichemsha supu, ukumbi wa Heartlands , Birmingham, Uingereza Jumamosi iliyopita. Makutano haya yalikuwa pia sehemu ya mchango mahususi kusaidia wasichana wanaopewa mimba kabla ya kuwa watu wazima, vijijini,  Arusha. Fedha zilikusanywa na mjasiria mali mkazi wa Birmingham, Mtanzania Sia Travel. Sia alijaa mlangoni akihakikisha kila senti iiliyolipwa na wahudhuriaji watashiba chakula ,  sanaa  usiku kucha na kuwafariji vigoli wetu, Tengeru.
(more…)

Read Full Post »

 

fab-moses-pic by f macha

Si wanamuziki wengi wanaoishi ughaibuni toka Bongo.  Miaka mingi hata hivyo  amekuwepo mtunzi na mwimbaji, Fab Moses ,  CD na shoo yake inayoitwa NENGUA.

Mtazame katika tovuti  ya My Space:

http://vids.myspace.com/index.cfm?fuseaction=vids.individual&VideoID=42998197

Mbali na nyimbo zake mathalani: “Ngunguri Ngangari” na “Nyerere” , Fab Moses huonekana katika majukwaa kadhaa ya London akitungua nyimbo mbalimbali za Kiswahili na bendi mashuhuri ya Afrika Jambo.  Bendi hii inasimamiwa na magwiji Kawele “Finger Printer”Mutimanwa, mpiga gitaa mashuhuri wa Kikongo, Uingereza na Ramadhani Athumani Mtunguja (“Rama Sax”) mpiga saxafoni mzawa wa Tanga aliyekuwa zamani na Simba wa Nyika na Les Wanyika na kushikiri katika kibao maarufu Sina Makosa kilichotolewa Nairobi mwaka, 1978. Afrika  Jambo hutumbuiza klabu kadhaa mashariki ya London zikiwemo (East Side Bar, Ilford) Kila Jumapili na Railway Tavern klabu ya Waganda, Forest Gate.

Waliomsikia Fab Moses huvutiwa na uzuri wa sauti yake inayokumbusha vibao mbalimbali vya nyumbani kama nyimbo za Shabani Marijani (Georgina), Simba wa Nyika, Mlimani Park, nk. Moja ya Sifa anazopewa Fab Moses ni sauti inayolandana sana na ya mwanasokomoko, hayati Marijani.

Mwanamuziki Fab Moses ni vile vile mwanasarakasi wa siku nyingi aliyeshafanya kazi na vikundi kadhaa nyumbani ikiwepo Muungano (cha Mzee Nobert Chenga) na Black Eagles. Kwa takribani miaka minane sasa anaongoza kikundi chake cha sarakasi na michezo jukwaani kinachoitwa Highflyers. Walioshamshuhudia (nikiwemo) wanakubali Fab Moses ni  mwalimu na kocha mzuri sana wa Sarakasi. Chini ya utaalamu wake mtu yeyote (watoto kwa wazima) anaweza kufundishwa kujinyonga nyonga na kuwa mwanasarakasi. Hilo latokana na uvumulivu na ufundi wake, Mtanzania huyu mwenye vipaji vingi…

fab-moses-singing

Habari zaidi za NENGUA, kikundi cha Sarakasi (Highflyers) au Afrika Jambo; mpigie Fab Moses -+44-7950-604530

Barua pepe: fabrahs@yahoo.co.uk

Picha na Freddy Macha

Read Full Post »