Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘WASATU’

 20180623_210120.jpg

Picha na Habari za Freddy Macha

 Kwa miaka mingi imesikika mikutano ya vyama na vilivyodai kushirikisha Watanzania Uingereza. Ila mwaka huu Jumuiya mpya iliyoundwa  (ATUK-” Association of Tanzania United Kingdom”)- imeahidi kuweka chombo tofauti.

(more…)

Read Full Post »

PICHA NA HABARI 

Za Freddy Macha

3-bango la WASATU

Jumuiya ya Wasanii Watanzania Uingereza (WASATU)  ilichemsha supu, ukumbi wa Heartlands , Birmingham, Uingereza Jumamosi iliyopita. Makutano haya yalikuwa pia sehemu ya mchango mahususi kusaidia wasichana wanaopewa mimba kabla ya kuwa watu wazima, vijijini,  Arusha. Fedha zilikusanywa na mjasiria mali mkazi wa Birmingham, Mtanzania Sia Travel. Sia alijaa mlangoni akihakikisha kila senti iiliyolipwa na wahudhuriaji watashiba chakula ,  sanaa  usiku kucha na kuwafariji vigoli wetu, Tengeru.
(more…)

Read Full Post »

 

Ukumbi wa The Eastern District Social Club, Northampton haujulikani kwa wengi. Hata hivyo eneo hili nje kidogo ya mji, ulijikuta ukikaanga Maandazi , Vitumbua na Nyama Choma punde Wasanii mseto wa Kitanzania walipozindua WASATU – jumuiya ya kuwakutanisha na kuwaunganisha. Ilikuwa Jumamosi 1 April, 2017.
Wimbo maarufu wa Les Wa Nyika, SINA MAKOSA, uliotungwa na Omari Shaaban, kuimbwa na Issa Juma na kupambwa gitaa maridadi la John Ngereza, ulikuwa kati ya vibao mbalimbali vya Kiswahili vilivyotukumbusha tukokako, na tu wapi, duniani. Umoja ni nguvu. Kiswahili oyee! Tanzania Oyee! Afrika Mashariki na Kati oyee!

Read Full Post »

 

9- Vitumbua vya Neema Kitilya

Jumuiya ya wasanii Watanzania Uingereza (WASATU)  ilizunduliwa kwa vigelegele na muziki mjini Northampton , katikati ya Uingereza jumamosi iliyopita. Tafrija hiyo ndogo lakini iliyowakutanisha zaidi ya Watanzania mia moja na marafiki zao wa Kenya, Uganda, Kongo , Nigeria, Uingereza nk, ilihudhuriwa na  Mheshimiwa Balozi Dk Asha Rose Migiro.

WASATU ilibuniwa mwaka jana kati ya wasanii wakiongozwa na mwanamuziki na mcheza sarakasi Fab Moses na promota wa vyakula vya Kitanzania, Bi Neema Kitilya.

Asilimia 20 ya kipato cha onesho  zilitolewa na WASATU kwa waliofikwa maafa ya mafuriko ya maji karibuni Tanzania.

1- Watanzania na marafiki zao wakijimwaga Northampton- pic by F Macha 2017

Watanzania na marafiki zao wakijimwaga ukumbi wa  The Eastern District Social Club, Northampton (more…)

Read Full Post »