Picha na Habari za Freddy Macha
Kwa miaka mingi imesikika mikutano ya vyama na vilivyodai kushirikisha Watanzania Uingereza. Ila mwaka huu Jumuiya mpya iliyoundwa (ATUK-” Association of Tanzania United Kingdom”)- imeahidi kuweka chombo tofauti.
Posted in Uncategorized, tagged ATUK, Balozi Migiro, Joe Warioba, JUmuiya, KSTL, Kwa Simu Toka London, Mkutano, Reading, Swahili Blogs, WASATU, Watanzania Ughaibuni, Watanzania Ulaya on June 27, 2018| Leave a Comment »
Picha na Habari za Freddy Macha
Kwa miaka mingi imesikika mikutano ya vyama na vilivyodai kushirikisha Watanzania Uingereza. Ila mwaka huu Jumuiya mpya iliyoundwa (ATUK-” Association of Tanzania United Kingdom”)- imeahidi kuweka chombo tofauti.
Posted in Uncategorized, tagged All Things African, Fab Moses, Fasihi ya Mwafrika, Hamida Mbaga, Jioni Ticha, KIswahili culture, Neema Kitliya, RamaSax, Saidi Kanda, WASATU, Watanzania London, Watanzania Ughaibuni, Watanzania Ulaya on May 8, 2018| Leave a Comment »
PICHA NA HABARI
Za Freddy Macha
Jumuiya ya Wasanii Watanzania Uingereza (WASATU) ilichemsha supu, ukumbi wa Heartlands , Birmingham, Uingereza Jumamosi iliyopita. Makutano haya yalikuwa pia sehemu ya mchango mahususi kusaidia wasichana wanaopewa mimba kabla ya kuwa watu wazima, vijijini, Arusha. Fedha zilikusanywa na mjasiria mali mkazi wa Birmingham, Mtanzania Sia Travel. Sia alijaa mlangoni akihakikisha kila senti iiliyolipwa na wahudhuriaji watashiba chakula , sanaa usiku kucha na kuwafariji vigoli wetu, Tengeru.
(more…)
Posted in Uncategorized, tagged Afrika Jambo, Fab Moses, Freddy Macha Videos, Les Wanyika, Nyimbo KIswahili, Sina Makosa, Swahili Music, WASATU on April 10, 2017| Leave a Comment »
Ukumbi wa The Eastern District Social Club, Northampton haujulikani kwa wengi. Hata hivyo eneo hili nje kidogo ya mji, ulijikuta ukikaanga Maandazi , Vitumbua na Nyama Choma punde Wasanii mseto wa Kitanzania walipozindua WASATU – jumuiya ya kuwakutanisha na kuwaunganisha. Ilikuwa Jumamosi 1 April, 2017.
Wimbo maarufu wa Les Wa Nyika, SINA MAKOSA, uliotungwa na Omari Shaaban, kuimbwa na Issa Juma na kupambwa gitaa maridadi la John Ngereza, ulikuwa kati ya vibao mbalimbali vya Kiswahili vilivyotukumbusha tukokako, na tu wapi, duniani. Umoja ni nguvu. Kiswahili oyee! Tanzania Oyee! Afrika Mashariki na Kati oyee!
Posted in Uncategorized, tagged Dk Asha- Rose Migiro, Northampton Tanzania, Swahili artists, Wasanii Afrika, Wasanii Tanzania, WASATU, Watanzania Uingereza, Watanzania Ulaya on April 8, 2017| Leave a Comment »
Jumuiya ya wasanii Watanzania Uingereza (WASATU) ilizunduliwa kwa vigelegele na muziki mjini Northampton , katikati ya Uingereza jumamosi iliyopita. Tafrija hiyo ndogo lakini iliyowakutanisha zaidi ya Watanzania mia moja na marafiki zao wa Kenya, Uganda, Kongo , Nigeria, Uingereza nk, ilihudhuriwa na Mheshimiwa Balozi Dk Asha Rose Migiro.
WASATU ilibuniwa mwaka jana kati ya wasanii wakiongozwa na mwanamuziki na mcheza sarakasi Fab Moses na promota wa vyakula vya Kitanzania, Bi Neema Kitilya.
Asilimia 20 ya kipato cha onesho zilitolewa na WASATU kwa waliofikwa maafa ya mafuriko ya maji karibuni Tanzania.
Watanzania na marafiki zao wakijimwaga ukumbi wa The Eastern District Social Club, Northampton (more…)