Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘Dk Asha- Rose Migiro’

Picha na Habari za Freddy Macha

1- Mhe Suluhu Samia akisalimiana na Dk Miohammed Hamza - pic by F Macha 2018Makamu wa Rais Mhe Suluhu Samia akizungumza na Dk Mohammed Hamza, kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Uingereza

Ulikuwa mkutano mfupi uliokusudia kutoa shukrani kwa wafadhili na Watanzania London wanaosaidia nyumbani. Fadhila hupitia Jumuiya ya Waingereza na Watanzania  (BTS) na kitengo chake cha TDT = shirika la Mfuko wa Maendeleo Tanzania.  BTS ilianzishwa mwaka 1975, na mlezi wake sasa hivi ni Rais mstaafu Ali Mwinyi.

BTS ilimkaribisha Makamu wa Rais Mheshimiwa Suluhu Samia, aliyekuja London wiki hii kudhuruia mkutano wa Viongozi wa Jumuiya ya Madola.

Kawaida viongozi hutegemewa  hotuba ndefu zenye maelezo yanayochosha masikio.

Mhe Suluhu alitua chuo kikuu cha lugha za Afrika na Mashariki ya Kati (SOAS)  akasalimiana na kupeana mikono na wananchi wa pande zote mbili. Hiyo tu ilitosha kuonesha imani yake kwa wananchi wachapa kazi wa pande hizi mbili.

2-Balozi Dk Asha Rose Migiro akizungumza na Kaimu Balozi Dar es Salaam Marc Thayre- pic by F Macha 2018Balozi wetu Uingereza, Dk Asha Rose Migiro akiwa na Kaimu Balozi Uingereza Tanzania, Mhe Marc Thayre

3- Dk Andrew Coulson mwenyekiti wa BTS aliyefungua na kufunga kikao- pic by F Macha 2018Mwenyekiti wa Jumuiya Ya Uingereza na Tanzania – BTS. Dk Andrew Coulson aliyefungua na kufunga kikao cha Brunei Gallery, SOAS.

4-Baadhi ya Watanzania waliohudhuriaBaadhi ya Watanzania waliohudhuria. Kutoka kushoto, Kiondo Wilkins, Dk Alex Paurine, Simon Mzuwanda na Joe Warioba
 

 

Read Full Post »

 

9- Vitumbua vya Neema Kitilya

Jumuiya ya wasanii Watanzania Uingereza (WASATU)  ilizunduliwa kwa vigelegele na muziki mjini Northampton , katikati ya Uingereza jumamosi iliyopita. Tafrija hiyo ndogo lakini iliyowakutanisha zaidi ya Watanzania mia moja na marafiki zao wa Kenya, Uganda, Kongo , Nigeria, Uingereza nk, ilihudhuriwa na  Mheshimiwa Balozi Dk Asha Rose Migiro.

WASATU ilibuniwa mwaka jana kati ya wasanii wakiongozwa na mwanamuziki na mcheza sarakasi Fab Moses na promota wa vyakula vya Kitanzania, Bi Neema Kitilya.

Asilimia 20 ya kipato cha onesho  zilitolewa na WASATU kwa waliofikwa maafa ya mafuriko ya maji karibuni Tanzania.

1- Watanzania na marafiki zao wakijimwaga Northampton- pic by F Macha 2017

Watanzania na marafiki zao wakijimwaga ukumbi wa  The Eastern District Social Club, Northampton (more…)

Read Full Post »

Picha  na habari za   Freddy Macha, London

Barabara ya Bond jijini London- pic by F Macha 2016

 Mwezi Julai Uingereza umekuwa wa vishindo vya kihistoria. Baba yao ni kujitoa Uingereza nje ya Jumuiya ya Ulaya (EU) na kuteuliwa Waziri Mkuu mpya mwanamke, Theresa May.

Kwa Watanzania, Uingereza mabadiliko ya mabalozi yalisikika.   Jumuiya ya Watanzania na Waingereza (British Tanzania Society) ilimkaribisha rasmi Dk Asha Rose Migiro na mwenzake mpya Tanzania, Bi Sarah Cooke. Bi Cooke aliyekuwa zamani Bangladesh alichukua nafasi ya Bi Dianna Melrose aliyesema aliwapenda sana Watanzania na lugha ya Kiswahili. (more…)

Read Full Post »