Feeds:
Posts
Comments

Posts Tagged ‘Balozi Asha Rose Migiro’

Picha na Habari za Freddy Macha

Hatimaye Watanzania Uingereza tumewachagua viongozi wa Jumuiya yetu ( Association of Tanzanians UK) yaani ATUK. Juni 2018 mkutano mkuu ulifanyika mjini Reading kufukuzia zoezi hili chini ya ulezi wa Balozi Mheshimiwa Asha Rose Migiro.
Mchecheto ulifukuzwa na wengi ila aliyewasha kiberiti alikuwa Joseph Warioba.
Baada ya mwaka, siku nzima ya Mtanzania, Jumapili 30 Juni , 2019, ilitayarishwa na wanakamati wa ATUK – ambao baadhi walikuja kuwa viongozi wa Jumuiya. Hapa inaonyesha namna juhudi za Balozi kutuunganisha zilivyoambatanika na ari na hamasa za Watanzania.
(more…)

Read Full Post »

Habari na Picha za Freddy Macha

TUMEZOEA kuwaita wenye hali hii “taahira” – neno la asili ya Kiarabu lenye maana “mtu asiye sawa” (wazimu, chizi, bwege, nk). Ila sahihi ni “mtindio ubongo” – kwa Kiingereza “Down Syndrome”….
(more…)

Read Full Post »

Picha na Habari za Freddy Macha

 

Kila mwaka wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, Ubalozi wa Tanzania huchagua usiku mmoja ambapo wananchi wa madhehebu yote hualikwa kufuturu.  Jumamosi 10 Juni, 2017 shughuli hii haikufanywa Ubalozini, wala haikuwa ya bure. Washiriki tulitakiwa kuchangia pauni 10 (kama shilingi 25,000) kutopoteza kodi za wananchi nje. Si kiasi kikubwa na kina mama nao walijitolea kupika na mikeka kukalia.

Pili,  mkutano wa takriban saa 3 na nusu uliwakutanisha Watanzania na Balozi Asha Rose Migiro kutathmini mada mbali mbali muhimu kabla ya kula. Desturi hii  ni ya kipekee kwa Watanzania na sijawahi kusikia ikifanywa na mataifa mengine. Zingatia pia kuwa kikao kilifanywa kanisa la Monravia, Hornsey kaskazini ya London.

(more…)

Read Full Post »

Picha na Habari za Freddy Macha, London

1-balozi-migiro-akihutubia-jumuiya-ya-watanzania-na-waingereza-pic-by-f-macha

 Balozi wetu Uingereza, mheshimiwa Dk Asha Rose Migiro alihutubia  jumuiya ya Watanzania na Waingereza (British Tanzania Society- BTS)  Jumamosi iliyopita. Hotuba hiyo iliyofanyika ukumbi wa Central Hall Westminster, London ni mara ya pili kwa balozi huyu mgeni kukutana na BTS. Mwezi Julai alikaribishwa rasmi akiwa na Balozi mpya Uingereza Tanzania Bi Sarah Cooke na aliyestaafu, Bi Diana Melrose.

8-bango-la-bts-pic-by-f-macha-2016

Mada hiyo iliyoitwa “Maendeleo ya Sasa Tanzania”  Ilikuwa sehemu ya mkutano wa 41 wa mwaka wa BTS na kuhudhuriwa na Watanzania na Waingereza wakazi hapa. (more…)

Read Full Post »