
Fikra za Umoja wa Waafika zilianza kuzungumziwa na kuchipuka kupitia Marcus Garvey- mwanarahakati wa Kijamaika aliyewasisimua viogozi wa mwanzo wa bara, miaka ya 1920 na 1930 . Garvey huzungumziwa sana katika Muziki wa reggae wa akina Bob Marley, Peter Tosh na Bunny Wailer. Alifariki na kuzikwa London mwaka 1940.

Marcus Garvey
Lengo lake mwandishi na mpiganaji huyu lilikua kuwaunganisha weusi wote duniani na kutupa moyo wa kujipenda na kutoogopa asilia yetu.
Continue Reading »
Posted in Uncategorized | Tagged Afrika Day, Afrika Jambo, BBC Swahili London, Charlton House, Global Fusion Music and Arts, Haile Selassie, Kawele Mutimanwa, Kwame Nkrumah, Marcus Garvey, Mwalimu Nyerere, Rama Sax, Salim Kikeke, Soma Cafe | Leave a Comment »
Wengi bado tuna imani kwamba matunda ni kitu cha nyakati fulani fulani na hasa kwa watoto wadogo tu.
Kumbe tunatakiwa tule matunda kila mara- ikiwezekana matano kwa siku. Kiongozi wake ni Parachichi.
Posted in Uncategorized | Tagged Chakula Bora, Maisha, Maisha Marefu, Maparachichi, Matunda na Afya, Parachichi, Uhai Wetu | Leave a Comment »
Imeandikwa na Freddy Macha
Picha zote na Urban Pulse

Mashabiki wakifurahia…
Kila mahali zilijazana foleni.
Za kuingia; kutokea, kununua vinywaji, kupata chips, nyama au vinywaji na za kuchangamkia majukwaa ya muziki na ngoma za Kiafrika. Ngoma hizo zilipigwa na bendi ya ACD Arts iliyoajiriwa na Hotel Marriott na wanamuziki mseto wa kijadi toka Uganda, Mali, Burkina Faso, Italia na Tanzania.

Wapiga ngoma wa- ACD Arts- mseto toka Uganda, Tanzania, Mali, Italia na Burkina Faso…
Continue Reading »
Posted in Uncategorized | Tagged ACD Arts, Africans in London, Bashir Rutasingwa, Frank Eyembe Fotos, Freddy Macha na Ngoma, Freddy Macha Twickenham, Hotel Marriotts, Ngoma za Tanzania, Ngoma za Uganda, Rugby 2013, Seby Ntege, Stephen Kasamba, Urban Pulse Fotos, Urban Pulse Twickenham | Leave a Comment »
Picha zote na F Macha

Wengi wetu tunaposikia “kufunga” fikra inayokuja kichwani ni mwezi Ramadhani na dini ya Kiislamu. Ukweli hapa Uzunguni ukisema “unafunga” jambo la kwanza unaloulizwa ni kama wewe Mwislamu, kwamba huli nguruwe na kadhalika. Kinachosahaulika ni kwamba dini mbalimbali zina tabia na mtindo wa kufunga na kutokula.
Ila mfungo ninaouongelea si wa kidini.

Madafu ni kinywaji kizuri sana- yanaweza kuchukua nafasi ya vinywaji vya makopo na chupa zenye sukari na chumvi zisizosaidia mwili. Kuna watu ambao bado wanasadiki na kuamini eti madafu husababisha ugonjwa wa kuvimba miguu au mbegu za uume! Duu makosa makubwa maana madafu yanaweza hata kukinga mambo hayo kwa madini na protini yake asilia!
Ni mfungo wa kusafisha, kupiga deki na kukarabati mwili.
Kawaida tunapokwenda haja kubwa – si kila kitu hutoka. Mabaki tumboni husongana kule kwa miaka hatimaye huanza kutuletea vidonda tumboni, harufu mbaya ya mdomo, ushuzi wa kutisha, maradhi kama saratani ya utumbo mkubwa nk. Njia moja ya kupunguza adha hii ni kutokula kwa saa 36 kuendelea.
Continue Reading »
Posted in Uncategorized | Tagged Chakula Bora, Chakula na afya, Elimu Afya, Freddy Macha na afya, Kitani, Kufunga, Kukarabati Mwili, Kuondoa unene, kupunguza unene, Mafuta ya Kitani- Flax Seed Oil, Nidhamu Binafsi, Pumzi na unene, Unene na Mazoezi, Uzuri wa Ngozi, Wajihi na Kula | Leave a Comment »

Oyster Card- ni kidude unachokiweka pesa (kama kadi tunazonunulia simu) ili kusafiri popote kwa basi au gari moshi jijini London. Ukiwa na pesa ndani yake usiposafiri-inakaa kama akiba hadi utakapoitumia. Kila unapoingia chomboni, unaigonga mlangoni karibu na dereva.
Duu…shauri ya baridi kali sasa hivi Majuu, wananchi wanakua na hamaki ya karibu. Jambo dogo hukumbusha kuku aliyehisi kuna mwewe au tai juu kumbe ni tawi tu la mti limetikisika…
Jana usiku nilikua natoka mazoezini.
Basi takribani tupu.

Baada ya vituo vitatu limeingia kundi la watu- nadhani walikuwa wanatoka shughuli moja kabambe maana ilikua kelele, harufu ya pombe na sigara- unajua fegi inavyopendwa nchi hizi za baridi… Kutokana na hali hiyo ya hewa- madirisha yote ya mabasi huwa yamefungwa kuhifadhi joto ndani.
Sasa…
Jamaa bila shaka wamestarahamika.
Hili neno nililisoma karibuni ndani ya riwaya mpya ya Profesa Said Ahmed Mohammed. Anaeleza maisha ya dada Hafida dunia ya Majuu (kaziita nchi hizi, Peponi). Hafida anaishi na shangazi yake anayemtesa sana. Sehemu fulani hadithini, mhusika anajiuliza maswali kuhusu dhiki na ubovu wa utajiri:
“Na nguvu hiyo inasimamia sitiari gani kama si pesa? Na pesa maana yake nini kama si ufunguo wa raha na starahamu? Pesa isiyopakwa wema ili kuzimua na kusafisha ukatili na uchafu wake,hiyo ni pesa?”
Starahamu.
Yaani kustarehe.
Neno adimu;…linaloweza kuwa tunu, kito au balghamu.
“Muhanga Nafsi Yangu” riwaya mpya ya Profesa Said Ahmed, mwandishi mahiri wa kisa bab kubwa- “Asali Chungu” 1976. Bado anaendelea kututumbiza kwa fasihi nta na sukari za Kiswahili fasaha. Wachapishaji wake ni Sasa Sema – Longhorn, Nairobi.
Msomaji, jamaa wanapanda basi wametoka zao starahamuni.
Msafiri kafiri kweli.
Sasa pale mlangoni lazima msafiri ugonge kadi yako hiyo ya malipo ( Oyster Card)… Kijana mmoja wa miaka ishirini na kitu ana simile zake ,bahati mbaya (au labda ni kutokujali ?), kamgonga kizee mmoja. Kibabu alikua akijivuta vuta, mosi ana mkongojo, mbili ana mizigo (katoka supamaketi kajaza mifuko ya vyakula), tatu hayuko sawa; ana kibiongo, mguu mmoja anaukokota, uso umejikunja kunja, mdomo umejikusanya kinamna; bila shaka ana maumivu si kidogo…
Kijana si kamgonga mzee wa watu?… nakisia kibabu ana miaka sabini na kitu.
Bidhaa za mzee zimedondoka. Kumbuka kuna kundi la “wastarahamika” linapenyeza penyeza; wengi na kwambia – kama kumi na kitu- kila mmoja ana hamasa na jazba za pombe, bangi na kadhalika. Tusisahau kusisitiza bangi ni kama “mahindi ya kukaanga” mji huu. Kama pua zako zinaitambua harufu yake- utaisikia kila kona na mtaa, mchana na usiku.
Mzee kadondosha bidhaa zake; watu wanataka kupita, kijana wala hana habari, kampita ajuza, wala samahani haikusikika, wala nini zaidi ? (wewe ungefanya nini hapo?….. huyooo, kiroboto kapanda zake juu ghorofani (ambapo vijana wengi hupahusudu). Ikabaki sasa wanasamaria wema kumsaidia babu.
Kule juu zinasikika kelele nyingi za fedheha, karaha na inzi.
Kijana anazozana na mmoja wa watu walioshuhudia kisa- mtu huyo hakupenda vile alivyompita ajuza bila hata kum-enzi kwa namna yeyote ile.
Twalisikia besi la kijana likinguruma na kupaaza mithili ya twiga mwenye tarumbeta:
“SHOW RESPECT TO ME AND I WILL RESPECT TO THE ELDERLY TOO.”
( “WAZEE KWANZA WANIONYESHE MIMI HESHIMA NDO’ NTAWAHESHIMU.”)
Duuu..wenzangu.
Somo hilo.
Hatimaye mzee wa watu alipata sehemu akakaa na mizigo yake. Na sikumsikia akinung’unika au kusema neno. Kule juu mvuke uliendelea kufoka hadi wakati nashuka kituo changu.
Hayawi hayawi huwa.

Basi la London- picha na F Macha
Posted in Uncategorized | Tagged Ajuza Uzunguni, Kiswahili Fasaha, Kizazi Kipya, Mabasi London, Msafiri Kafiri, Muhanga Nafsi Yangu, Mwandishi Said Ahmed Mohammed, Sasa Sema -Longhorn Publishers, Staharamu, Vituko vya London, Wazee na Vijana Ulaya | Leave a Comment »

Mabasi mekundu ya London yamekuwepo toka mwaka 1829, yalipoundwa na mbunifu George Shillibeer. Enzi hizo za madongo kuinama yalikuwa yakivutwa kwa farasi. Umashuhuri wake haukuanza leo.
Moja ya hadithi zangu ndani ya kitabu “Mpe Maneno Yake” (E & D Limited, 2006) zinaelezea namna wakazi wa Dar es Salaam wasivyokuwa na subira pale abiria mwenzao (au kondakta na dereva) anapokosea. Kisa cha “Mpe Maneno Yake” kilitokea mwaka 1979- lakini sidhani hali imebadilika. Hala hala na hisia kali za wasafiri ni zile zile.

Nilipoandika wakati huo bado kijana- nlidhani haya ni mambo ya Tanzania na Afrika tu. Lakini yamo miji mikubwa mikubwa yote duniani. Baada ya kusafiri miaka mingi nimegundua wakazi wa miji mikubwa wote kabila moja tu.
Leo usiku nilikua natoka mazoezini, nimelowana kijasho jasho, basi halikua na abiria wengi. Ilikua takribani saa 4 na kitu usiku. Hali tulivu, lelemama hamna.
Ghafla dereva wa basi badala ya kupitia njia inayotakiwa kapitiliza. Yalikua makosa. Abiria wote gaaaaaaa.
Lakini naye dereva kang’amua; akasimamisha basi, kati kati ya barabara. Sasa nsikilizie vurumai.
Continue Reading »
Posted in Uncategorized | Tagged Dar es Salaam, E & D Limited Tanzania, Fasihi ya Miji, Hamaki na Mahusiano, Mabasi London, Maisha ya Mijini, Mawasiliano, Mazingira na Miji, Miji na Hisia, Mpe Maneno Yake, Twen'zetu Ulaya, Uandishi Kiswahili, Usafiri, Utamaduni Abiria, Waandishi Kiswahili | 6 Comments »



